Monday, September 30, 2013

NIA YA ZITTO KABWE JUU YA KUFANYA MAREKEBISHO YA SHERIA YA MAGAZETI.

Nimetoa taarifa rasmi kwa katibu wa Bunge kwa mujibu wa kanuni za Bunge kwamba katika mkutano ujao wa Bunge nitawasilisha muswada binafsi wa sheria kufanya marekebisho ya sheria ya magazeti kwa lengo la kuifuta kabisa sheria hiyo.
Madhumuni ya muswada huo ni;

“kufuta sheria ya magazeti ya mwaka 1976 kwa sababu inakizana na Katiba ya Nchi kuhusu haki za Raia kupata habari na kwamba iliorodheshwa na tume ya Nyalali ni sheria kandamizi’
...
Muswada wenyewe nitauwalisilisha siku ya ijumaa ili uchapwe kwenye gazeti la Serikali uweze kuingia kwenye shughuli za Bunge zitakazoanza tarehe 15 Oktoba 2013 kwa ngazi ya kamati.

September 30, 2013
Source : Zitto social media.

JOB VACANCIES - NELSON MANDELA AFRICAN INSTITUTE OF SCIENCE & TECHNOLOGY.

YANGA - TAARIFA KUHUSU MRADI WA UWANJA.

Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini Francis Kifukwe (katikati) ambaye pia ni mwenyekiti wa mradi wa ujenzi wa uwanja eneo la jangwani akiongea na waandishi wa habari makao makuu ya klabu leo, kushoto ni mzee Jabir Katundu (mwenyekiti wa baraza la wazee) na kulia Lawrence Mwalusako katibu mkuu wa Yanga SC
 
LEO tungependa kupitia kwenu kutoa taarifa kuhusu maendeleo ya mradi wetu wa Uwanja wa kisasa wa mpira katika Jiji la Jangwani kama itakavyojulikana

Mara ya mwisho tuliongea ama kuonana ilikuwa mwezi wa tatu wakati Ndugu zetu wa BCEG walipokabizi Concept design ama Usanifu wa awali na kuanzia sasa tutakuwa tunatoa taarifa za mara kwa mara kuhusu mradi huu. Wahenga walisema UKICHA KUSEMA HUTATENDA JAMBO lakini pia KUKAA KIMYA SANA kunajenga hisia mbaya na kutoa nafasi ya upotoshwaji wa habari. 

Kwa kifupi napenda kuwakumbusha kuwa Makubalino ya Awali (Memorandum of Understanding) yalisainiwa 23 Novemba 2012. Pamoja na mengineyo YANGA inatakiwa:
Kupata na kuwa na eneo la kutoshereza malengo ya mradi
Kupata ushauri mzuri, michoro mizuri na mkandarasi mzuri wa mradi
Kupata na kutenga fedha za kukamilisha usanifu na ujenzi wa mradi

Kwa upande wa BCEG wajibu wao ni kuwa na utaalamu na uzoefu wa kutosha. BCEG wameandaa na kukabidhi michoro ya usanifu wa awali kukidhi matakwa ya YANGA. YANGA tunatakiwa kutoa maoni yetu na na kuingia RASMI mkataba wa ujenzi.

Kutokana na kukua kwa Jiji la Dar es Salaam, na katika hali ya kutaka klabu iwe na vitega uchumi klabu imeonelea ni vyema kama ingekuwa na uwanja wa mpira wa karne ya sasa na baadaye ambao pamoja na mambo mengine utakuwa na mioundombinu ifuatayo:-

Mahojiano na Katibu Mkuu wa CHADEMA Dr. Willbrod Slaa _ MAREKANI

EMPLOYMENT VACANCIES - PCCB.

EMPLOYMENT VACANCIES
The PCCB is an Independent Public Institution and law enforcement Agency established by Section 5 of the Prevention and Combating of Corruption Act No. 11 of 2007. The Bureau is mandated to carry out three major functions: Prevention, Community Education and law enforcement in Tanzania mainland.
Suitably qualified Tanzanians are invited to join our family in the following positions:

1.0 INVESTIGATION OFFICERS (214 POSTS)
1.1   DIRECT ENTRANTS (FROM COLLEGES/UNIVERSITIES)
  • Applicants should posses three years Advanced Diploma or Undergraduate degree from recognized higher learning Institutions in any of the following fields: Quantity survey, Accountancy, Human Resources Management, Law, Procurement, Journalism, Information Technology, Highways Engineering, Building Constructions, Electrical Engineering, Land Management and Valuation, and Forensic Knowledge.

JOB OPPORTUNITY IN TANZANIA.

Climate Change

Job Opportunity Energy Efficiency Expert (National)
Posted on 17 Sep, 2013
Application by 8 Oct, 2013
Project Status: Tender
Project Title Sustainable use of Renewable Energy - Component: Promotion of Energy Efficiency
Period of Project: Feb, 2014 - Dec, 2016
Duration of assignment:35 months
Country:Tanzania
Duty Station:to be determined
Job Code AFR-TZA13GIZ0232/2

Project Description: The goal of the program (target module) is: The conditions for the sustainable use of Renewable Energy (RE) are improved in Tanzania. The program supports the expansion of grid-connected renewable energies through advisory on the general framework and capacity building. The procedures for approval of small RE systems (10 MW), which are supported through the Rural Energy Agency REA, should be organized more efficiently. In addition, strategies and support measures for Energy Efficiency are supported. Political support is the Ministry of Energy and Minerals (MEM).

Job Description:Subject to this tender is the "promotion of energy efficiency (EE)".

Key tasks include:

  • Promotion of energy efficiency
  • Technical design and economic analysis of pilot projects 
  • Design of measures for the promotion of EE
  • Technical audits/energy audits
  • Organization of workshops and awareness raising campaigns


Qualifications:
  • Master degree or equivalent diploma in engineering, economics or other relevant sector
  • Specific technical and economic knowledge in the field of energy supply and utilization as well as energy efficiency
  • Expertise in the above mentioned topics
  • At least 5 years working experience in the promotion of energy efficiency
  • Extensive knowledge of the Tanzania energy sector and its institutions
  • Working knowledge of English and Swahili
  • Excellent communication skills
  • Proven project management skills
  • Full command of Microsoft Office software

CV-Form: CV GIZ

Contact Person: Romy Rösner
Contact: Roesner@gfa-group.de

Wigh Fellowships for International Scholars at Harvard University in USA, 2014

Weatherhead Center for International Affairs through the Weatherhead Initiative on Global History (WIGH) offers fellowships for international scholars in the USA. The fellowships are available to support outstanding scholars whose work respond to the growing interest in the encompassing study of global history. Applications are welcomed from qualified persons without regard to nationality, gender, or race. Fellows will receive an annual stipend of up to $50,000, according to fellows’ needs. WIGH Fellows are appointed for one year and are provided time, guidance, office space, and access to Harvard University facilities. Applications should be submitted till January 10, 2014.

Friday, September 27, 2013

Wakuu wa usalama kuhojiwa Kenya.


Maafisa wakuu wa ujasusi wametakiwa kufika mbele ya kamati ya ulinzi ya bunge ili kuhojiwa kuhusu mashambulizi ya kigaidi dhidi ya jumba la Westgate mjini Nairobi.
Taarifa kwenye vyombo vya habari nchini humo zinaonyesha kuwa hali ya kulaumiana imeanza kuibuka huku mashirika ya usalama yakinyosheana kidole.

Watu 67 waliuawa kwenye shambulizi hilo huku zaidi ya miamoja sabini na tano wakipata majeraha mabaya. Shirika la Red Cross nalo linasema kuwa watu 61 wangali hawajulikani waliko.
Wataalamu wa uchunguzi wa mauaji wangali wanafanya uchunguzi wao wakitafuta miili na dalili za kilichosababisha shambulizi hilo.
Kamati ya bunge inataka maafisa wanaohusika na maswala ya usalama waweze kuwajibishwa.
Kundi la kigaidi la nchini Somalia, al-Shabab limedai kufanya mashambulizi hayo yaliyodumu siku nne kama hatua ya kulipiza kisasi kwa Kenya kujihusisha nchini Somalia kijeshi.
Hii leo ni siku ya tatu ya maombolezi kwa wathiriwa wa shambulizi hilo wakiwemo raia na wanajeshi.
Rais Uhuru Kenyatta amehudhuria mazishi ya mpwa wake na mchumba wake mjini Nairobi ambapo aliwahutubia waumini.

Walipuuza onyo?

Hatua ya kuwataka maafisa hao wa usalama kufika mbele ya tume ya bunge siku ya Jumatatu, inakuja kutokana na wasiwasi miongoni mwa wakenya kuhusu kiwango cha maafisa hao kujiandaa kwa tukio lolote la kigaidi sawa na lililotokea Westgate.
Kwa mujibu wa vyombo vya habari mmoja wa maafisa waliotakiwa kufika mbele ya kamati hiyo ni mkuu wa shirika la ujasusi Michael Gichangi, anayesema alitoa taarifa za ujasusi kuhusu shambulizi hilo kwa polisi.
Lakini, afisaa mmoja mkuu katika idara ya polisi alikana kuwa taarifa hiyo ilitolewa kwa polisi.

Chanzo: BBC

KIFO CHA MWANDISHI WA HABARI WA MWANANCHI VENANCE GEORGE.

Marehemu Venance George.
Mwandishi wa habari wa Mwananchi Communication Limited Venance George, jana alipoteza maisha akiwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro alipokuwa amelazwa.
Marehemu alikuwa akisumbuliwa na vidonda vya tumbo kwa muda mrefu na kifua hali iliyopelekea kwenda kulazwa katika hospitali ya Aga Khan iliyopo jijini Dar es salaam na kupata nafuu, Baada ya kurudi nyumbani hali ilbadilika tena na kupelekea kwenda kulazwa katika hospitali ya Holly Cross Mission iliyopo mkoani Morogoro na baadaye kuhamishiwa katika hospitali kuu ya mkoa wa Morogoro.

Marehemu alipata nafuu na kuruhusiwa kurudi nyumbani , baada ya siku kadhaa hali ilibadilika tena na kupelekea kwenda kulazwa hospitali ya mkoa wa Morogoro hadi umauti ulipomkuta mnamo tarehe 26/09/2013 saa 9:15.
-Marehemu ameacha mjane na watoto wawili wa kike na wa kiume.
 
HISTORIA FUPI YA MAREHEMU VENANCE GEORGE.
Marehemu Venance George Mhangilwa alizaliwa mnamo 8/12/1973 Bukoti wilaya ya Geita.
ELIMU:
-Marehemu alisoma katika shule ya msingi Bugogo kuanzia mwaka 1981 mpaka mwaka 1987 alipohitimu elimu yake ya msingi.

-Mnamo mwaka 1988 alianza kidato cha kwanza katika shule ya sekondari Forest Hill iliyopo Morogoro na kuhitimu kidato cha sita mnamo mwaka 1994.
-Mwaka 1995 alijiunga katika chuo cha uandishi wa habari na kuhitimu mwaka 1996.
AJIRA:
Marehemu alianza kazi ya uandishi wa habari katika kampuni ya,
 -Uhuru Publication Limited, 1996-1998.
-Kuna Entarprises Company Limited, 1998-1999.
-Village Travel And Transport Project (VTTP), 2001-2003.
-Swiss-Contact Tanzania Limited, 2001-2003
-Mwananchi Communication Limited, 2003 mpaka mauti yalipomkuta.
Pia alijiendeleza kimasomo katika chuo kikuu huria cha Tanzania ambapo alitakiwa kuhitimu shahada yake ya mawasiliano ya umma mwezi wa 12 mwaka huu 2013.

Monday, September 16, 2013

ZITTO KABWE AKIHOJIANA NA MAMA ALIYEDAIWA KUWA MUHAMIAJI HARAMU KUMBE SIO.

"Mama huyu kakamatwa kama mhamiaji haramu na kupelekwa Ubalozi mdogo wa DR Congo uliopo Manispaa ya Kigoma. Amezaliwa Tanzania, amesomea Tanzania, Baba yake Mtanzania, Babu yake Mtanzania na Ndugu zake wengine Watanzania na hawakukamatwa. Amekamatwa akitoka kuchota maji ziwani Tanganyika. Malalamiko yake nimeyafikisha kwa Waziri wa Mambo ya Ndani".
Chanzo: Zitto Social media.

VIBONZO VILIVYOIKUNA BLOGU HII.



Friday, September 13, 2013

UNAIKUMBUKA ZE COMEDY YA MAPOUDA? HII HAPA Dawa ya Mapenzi

Postgraduate Research Scholarships at La Trobe University in Australia, 2014.

La Trobe University offers postgraduate research scholarships in Australia. In 2014 La Trobe University will award over 150 living allowance scholarships to candidates enrolling in Doctoral and Masters by research programs and approximately 40 fees awards to meet tuition costs for international students. The closing date for applications is 31 October 2013 for Australian and New Zealand citizens and 30 September 2013 for overseas applicants.
Study Subject(s): While applications are open to any area of study, La Trobe University would be particularly interested in applications within the research focus areas of: Building Healthy Communities, Securing Food, Water and the Environment, Sport, Exercise and Rehabilitation, Transforming Human Societies and Understanding Disease
Course Level: Scholarships are available for postgraduate students who are undertaking higher degrees by research at La Trobe University.
Scholarship Provider: La Trobe University
Scholarship can be taken at: Australia
Eligibility: -La Trobe University’s postgraduate research program includes Doctoral and Masters degrees by research.
-Applicants for Doctoral candidature should have completed an Honours Bachelor degree at a very high level of achievement or
already hold a Masters degree.
-Applicants for Masters by research candidature are usually required to have completed an Honours degree or Masters Preliminary.
-Prospective local applicants for Doctoral and Masters by research degrees should contact the Faculty in which they wish to study
to ascertain the availability of supervision and to obtain an application kit.
-International students should contact the La Trobe International Office or visit the University’s International web site for
information about application procedures and study opportunities at La Trobe University.

J.MARTINS KUWASHA MOTO USIKU WA LEO NDANI YA ELEMENTS LOUNGE.


VACANCIES FOR VOLUNTEERS HLSSF.

KNOW YOUR ADMISSION THROUGH TCU 2013/2014 IN DIFFERENT UNIVERSITIES.

SEARCH FOR YOUR ADMISSION HERE

Application Form for Thailand Scholarship.

Announcement for Thailand International Postgraduate Programme (TIPP) for the Year 2014.

SELECTED STUDENTS IN DEGREE PROGRAMS - WATER INSTITUTE.

ANNOUNCEMENT- CHANGE OF BANK ACCOUNT NUMBERS DIT.

J. MARTIN NA A.Y KUSHIRIKIANA NA VODACOM WALIPOTOA MISAADA KWA WATOTO YATIMA DAR JANA.

Wanamuziki nguli Justice Martince (J.Martins) Kutoka nchini Nigeria na Ambwene Yessaya (AY) wakitoa misaada kwa watoto yatima wa kituo cha Chamanzi Yatima Trust Fund kwa ushirikiano na kampuni ya Vodacom, wasanii hao walitoa wito kwa wasanii wengine kujitolea kuwasaidia watoto waishio katika mazingira magumu.

Msanii nguli wa muziki kutoka nchini Nigeria Justice Martins, (J.Martins) akizungumza na watoto waishio katika mazingira magumu (Hawapo pichani) wa kituo cha kulelea watoto yatima cha Chamanzi Yatima Trust Fund, walipo watembelea na kutoa misaada mbalimbali kwa watoto hao. Pamoja nao katika picha (waliokaa) ni wafanyakazi wa Vodacom, alie simama ni msanii Ambwene Yessaya. (AY).

Msanii nguli wa muziki kutoka nchini Nigeria Justice Martins, (J.Martins) akizungumza na Mkuu wa Kitengo cha huduma za jamii cha Vodacom, (Vodacom Foundation) Yessaya Mwakifulefule na Mlezi wa kituo hicho Bi. Winfrida Lubanza wakati wa utoaji wa misaada kwa watoto wanaolelewa katika kituo cha watoto yatima cha Chamanzi Yatima Trust Fund. Pamoja nao ni Meneja wa Chapa wa Vodacom Tanzania, Nicholous Machugu.


Msanii nguli wa muziki kutoka nchini Nigeria Justice Martins, (J.Martins) akizungumza na waandishi wa habari (Hawapo pichani) wakati wa utoaji wa misaada kwa watoto waishio katika mazingira magumu wa kituo cha Chamanzi Yatima Trust Fund.

National Scholarship Programme for Foreign Applicants in Slovak Republic, 2013/14.

Applications are invited for National Scholarship Programme for summer semester of the academic year 2013/14. The National Scholarship Programme of the Slovak Republic supports study/research/teaching/artistic mobility of foreign students, PhD students, university teachers, researchers and artists at universities and research organisations in Slovakia. The scholarship shall cover scholarship holders’ living costs (accommodation, board, etc.) during their study/research/teaching/artistic stay. The application deadline is 31 October 2013.
Study Subject(s): Scholarships are provided to learn any of the courses offered by the universities and research organisations in Slovakia.
Course Level: The National Scholarship Programme of the Slovak Republic supports study/research/teaching/artistic mobility of foreign students, PhD students, university teachers, researchers and artists at universities and research organisations in Slovakia.
Scholarship Provider: The Ministry of Education, Science, Research and Sport of the Slovak Republic
Scholarship can be taken at: Slovak Republic
Eligibility: The following individuals are eligible applicants for a scholarship in the framework of the NSP:
A) students, who are university students abroad and will be participating on a study stay in Slovakia within their 2nd level of higher education (or will be participating on a study stay in Slovakia at least during the 7th semester of their higher education, i.e. in case that they are students of a joined study programme – joined 1st and 2nd level of higher education), and who are accepted by a public, private or state university in the Slovak Republic to an academic mobility  to study in the Slovak Republic;
B) PhD students, whose higher education or research preparation takes place abroad, and who are accepted by a public, private or state university or research organisation eligible to carry out a PhD study programme2 (e.g. Slovak Academy of Sciences) in the Slovak Republic to an academic mobility1 to study/conduct research in the Slovak Republic;
C) foreign university teachers, researchers or artists, who are invited by an organisation with a valid certificate of competence to carry out research and development seated in the Slovak Republic, and which is not a business organisation3 to a teaching/research/artistic stay in the Slovak Republic.

ADMITTED STUDENTS 2013/14 JoKUCo

Thursday, September 12, 2013

UMOJA WA MATAIFA YAIKOSOA TANZANIA KWA KUWAFUKUZA WAKIMBIZI


Umoja wa Mataifa umesema kuwa takriban wakimbizi elfu 25 kutoka Burundi wameondoshwa Tanzania kwa nguvu katika mwezi mmoja uliopita.
Afisa wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuwahudumia wakimbizi amesema malori yanayowasafirisha warundi yamekuwa yakivuka mpaka kila siku , huku wakimbizi wengi wakikosa mahitaji muhimu kama vile maji na chakula .
Katika wiki za hivi karibuni, Tanzania imekuwa ikiwafukuza wakimbizi kutoka Burundi, Rwanda na Jamuhuri ya Kidemokrasi ya Kongo .
Kwa miaka mingi Tanzania iliwahifadhi mamilioni ya wakimbizi waliokuwa wakiyakimbia mapigano katika nchi jirani .

Takriban watu milioni moja walitoroka kutoka Burundi na kuingia Tanzania wakati wa mgogoro wa wenyewe kwa wenyewe wakati vita vilipozuka mwaka 1993. Wengi walirejea kwa hiari wakati amani ilipopatikana mwaka 2006.
Lakini inaonekana Tanzania haina tena uvumilivu kwa swala hilo. Nchi hiyo imekuwa makao kwa mamilioni ya wakimbizi katika kipindi ya zaidi ya miaka kumi iliyopita kutokana na migogoro katika eneo la maziwa makuu.
Maafisa sasa wameanza kupiga jeki juhudi za kuwaondoa wakimbizi hao kutoka Burundi, Rwanda, na Jamuhuri ya kidemokrasia ya Congo kwa nguvu wakiwataka kurejea makwao.
Tanzania inasema kuwa wakimbizi hao ni wahamiaji haramu.
Shughuli hii imetokea wakati mmoja na mgogoro wa kidiplomasia kati ya Tanzania na Rwanda ambayo imekuwa ikikanusha madai ya kuchochea vurugu katika Jumuhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
Mgogoro ndani ya Jamuhuri ya kidemokrasia ya Congo nao unaendelea kuchochea idadi ya wakimbizi wanaotoroka vita na kuingia katika nchi jirani.

Chanzo: BBC

ALICHOKISEMA DIAMOND BAADA YA "VODACOM NGOLOLO CHAT" MCHANA WA LEO.

University of Waikato Doctoral Scholarships for International Students in New Zealand, 2014.

University of Waikato is offering doctoral scholarships for domestic and international applicants. All applicants must have submitted an application to enroll for doctoral studies at the University of Waikato prior to, or at the same time as, applying for a Doctoral Scholarship. The total value of a scholarship shall be a living allowance of up to $22,000.00 per annum (pro rata for part-time candidates) and an amount equal to the annual tuition fees payable during the term of the Scholarship. The application deadlines are 31 October 2013 (for Round 1) and 30 April 2014 (for Round 2).
Study Subject(s): Scholarships are provided to learn any of the courses offered by University of Waikato in New Zealand.
Course Level: These scholarships are available for pursuing postgraduate research level at University of Waikato in New Zealand.
Scholarship Provider: University of Waikato, New Zealand
Scholarship can be taken at: New Zealand
Eligibility:
-University of Waikato Doctoral Scholarship is open to domestic and international applicants.
-All applicants must have submitted an “Application to enroll for doctoral studies at the University of Waikato prior to, or at the same time as, applying for a Doctoral Scholarship. Scholarship applications will only be selected for consideration once the applicant has received an Offer of Place for Doctoral study at the University of Waikato.
-Candidates already enrolled in a doctoral degree at the University of Waikato may apply. However, the Selection Panel will favour applications from new doctoral students and of those; preference will be given to applicants who have completed the entry qualifications for doctoral study. Scholarships (of reduced duration) may be offered to a candidate who has been enrolled in doctoral studies for six months full-time, or twelve months part-time, or more.

VODACOM NA BENKI POPOTE HII HAPA.

Fanya miamala ya kibenki bila ya kubanduka ulipo. Piga *150*00# na Chagua huduma za kifedha.

JOB VACANCIES - UDSM.

JOB VACANCIES - DAWASCO.

 
PURPOSE STATEMENT

DAWASCO is a Public Corporation which was established to provide water and sewerage services to the City of Dar Es Salaam and some parts of Coast Region. It has vacancies which has to be filled immediately.

Applications are now invited from suitable internal candidates to fill in the position of Finance Manager, Plant Manager, and Plant Operations Supervisor.

POSITION:       FINANCE MANAGER (1 Post)

CORE FUNCTIONS

The Finance Manager shall   be responsible in assisting Chief Finance Officer in accounting for the revenue and expenditure of the Corporation
  
Reporting:
Shall be reporting to Chief Finance Officer

Main Duties and Responsibilities

·         Produce the weekly financial statements and monthly management accounts.
·         Produce the management accounts for Board meetings
·         Monitor actual performance Vs budget
·         Make monthly projections of Revenue Expenditure Budget
·         Authorise suppliers’ invoices for payment
·         Authorise payments to creditors
·         Keep various books of accounts as per IFRS
·         Ensure compliance of the PPRA 2004
·         Supervise subordinates to conform with laid down financial policies and regulations Bachelor of Finance and Accounting/Accountancy

Qualification and Experience
The Ideal Candidate must possess a Bachelor of Commerce (Finance, Accounting), holder of CPA or similar positions must be registered as a practitioner.

Competencies
The holder of the position should be able to apply knowledge, skills and understanding in a wide and unpredictable variety of contexts with substantial personal responsibility, responsibility for the work of others and responsibility for the allocation of resources, policy, planning, execution and evaluation

Salary and Remuneration

 competitive salary as per DAWASCO scheme and benefits will be offered to the right candidate.
 

POSITION:       PLANT MANAGER    (2 Posts)


LEO NI LEO LIVE NA DIAMOND NDANI YA "VODACOM NGOLOLO CHAT" SAA 8 MCHANA.

 
Ongea live na Diamond Platnumz leo saa 8 mchana katika ukurasa wa Facebook na Twitter wa Vodacom. Kama una swali lolote tafadhali usikose kujiunga nao leo.

Wednesday, September 11, 2013

Transform Together Scholarships for International Students at Sheffield Hallam University in UK, 2014.

Sheffield Hallam University offers Transform Together Scholarships for International Students in UK. Scholarships are open to students from any non-EU country applying to study at Sheffield Hallam University to enrol in the 2013/14 academic year. All full-time postgraduate and undergraduate taught courses are eligible. The scholarships include a one-year full tuition fee waiver for full-time taught postgraduate courses and 50% tuition fee discount for each year of an undergraduate course (subject to successful progression). The application deadline is 1st November 2013.
Study Subject (s): All full-time postgraduate and undergraduate taught courses are taking part in the programme at Sheffield Hallam University.
Course Level: Scholarships are available for pursuing postgraduate and undergraduate taught degree level at Sheffield Hallam University.
Scholarship Provider: Sheffield Hallam University
Scholarship can be taken at: UK
Eligibility: To be eligible to apply for one of these scholarships you must be:
-postgraduate only – have achieved a minimum 2.1 or equivalent in your honours degree and must meet the minimum course entry requirements. Please attach transcripts to scholarship applications.
-undergraduate only – you must achieve or exceed the entry criteria for the course.
-have an unconditional/conditional offer to study a full-time postgraduate course at Sheffield Hallam University.
-be enrolling on a one year full-time taught postgraduate course with Sheffield Hallam starting in the 2013/14 academic year
-be self-funding your studies
-have, or expect to achieve, a minimum of IELTS 6.0 (5.5 in all areas) or equivalent*
-be classed as an international student for fees purposes
-be able to pay any additional fees your course may require, for example field trips

WALIOPANGIWA VITUO VYA KAZI WIZARA YA AFYA AWAMU YA III.

WALIOPANGIWA VITUO VYA KAZI WIZARA YA AFYA AWAMU YA III

DR. SLAA KUNGURUMA WASHINGTON DC - MAREKANI.


Tuesday, September 10, 2013

1st BATCH SELECTED CANDIDATES NACTE 2013/2014 OUT.

TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA KWA MADAKTARI, MADAKTARI WA MENO, TABIBU, TABIBU WASAIDIZI NA WATAALAMU WA MAABARA

Norwegian Government Quota Scheme for Eastern European, Developing & Central Asian Countries, 2013/14.

Norwegian Government offers Quota Scheme for Developing Countries’ Students in Norway. The scheme normally includes courses taught in English at Master’s and PhD level, in addition to certain professional degrees at selected Norway Universities. The Quota Scheme will only enrol students from institutions (organisations, universities, authorities) which have collaboration agreements with Norwegian universities or colleges. Norwegian institutions usually do not admit free movers (individual applicants) to this scheme. Only in very special cases will free movers be considered. The deadline for applications for the Quota scheme is usually 1st December every year.
Study Subject (s): Scholarships are provided to learn any of the courses offered by the Selected Norway Universities.
Course Level: The scheme normally includes courses taught in English at Master’s and PhD level, in addition to certain professional degrees at Selected Norway Universities.
Scholarship Provider: Norwegian Government
Scholarship can be taken at: Norway
Eligibility: -The Quota Scheme will only enrol students from institutions (organisations, universities, authorities) which have collaboration agreements with Norwegian universities or university colleges. Norwegian institutions usually do not admit free movers (individual applicants) to this scheme. Only in very special cases will free movers be considered. Please contact the institutions directly for individual information.
-Students who come to Norway as self-financing students will, as a rule, not be considered as being qualified for the Quota Scheme.
-Students usually apply for degree programmes that serve as a continuation of their studies in their home country or for courses which can be a joint part of a degree programme in their home country (joint degree or sandwich programmes). Most of the programmes offered are at Master’s or PhD level, but the Quota Scheme also offers certain Bachelor’s study programmes.

Monday, September 9, 2013

SHEIKH AKAMATWA KWA KUBAKA MOROGORO.

Sheikh wa Msikiti wa MasjidMaftah Mjini Morogoro amekamatwa na Polisi kwa tuhuma za kumbaka mtoto wa miaka nane (8) nyumbani kwake.
Habari zaidi tutazidi kuwaletea kadiri tutakavyokuwa tunazipata.

TANGAZO LA SKOLASHIPU ZILIZOTOLEWA NA SERIKALI YA SRI LANKA KWA TANZANIA KWA MWAKA 2013/2014.

Serikali ya Tanzania imepokea mwaliko wa Skolashipu kutoka kwa Serikali ya Sri-Lanka kwa mwaka 2013/2014.

Wadau wote, raia wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, wenye sifa wanashauriwa wasome mwongozo na fomu za maombi kwenye Kiambatisho cha tangazo hili na kuyafanyia kazi.

Maombi yaliyokamilika yakiwa na nyaraka zote zilizoorodheshwa kwenye Kiambatisho yawasilishwe Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kabla ya tarehe 15/09/2013 kwa anuani ifuatayo:-

Katibu Mkuu,
Wizara Ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi,
S. L. P 9121,
DAR ES SALAAM

JOB ADVERTISEMENT - POSTAL BANK SEPTEMBER 2013.

Rais JK aonja nguvu ya CHADEMA Mwanza.

ISHARA YA VIDOLE VIWILI, PEOPLES POWER VYATAWALA
RAIS Jakaya Kikwete jana alipata wakati mgumu, baada ya kukutana na nguvu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) jijini Mwanza katika ziara yake, huku Waziri wake wa Ujenzi, Dk. John Magufuli, naye akijikuta akizomewa mbele yake.
Mbunge wa Nyamagana, Ezekia Wenje, alivunja mwiko baada ya kujiunga katika msafara huo wa raia akiwa na gari lenye alama za Movement for Change (M4C) lililokuwa limefungwa bendera mbili za CHADEMA.
Hata hivyo maofisa usalama walipata wakati mgumu kulizuia gari hilo lisiwepo katika msafara huo, jambo lililozua tafrani kidogo katika uwanja wa Furahisha ambapo Kikwete alikuwa akihutubia mkutano wa hadhara.
Awali wakati wa uzinduzi wa wodi ya wazazi iliyoko eneo la Butimba, Rais alilazimika kumpa Wenje nafasi ya kuwasalimia wananchi baada ya Mkuu wa Mkoa, Evarist Ndikilo, kutaka kufanya hila ya kumnyima haki hiyo kama mbunge wa jimbo husika.
Baada ya viongozi wote kutambulishwa bila Wenje kutajwa, wananchi walianza kupaza sauti wakitaka mbunge wao naye atambulishwe.
Wenje baada ya kusimama alimshukuru Rais Kikwete kwa kumpa nafasi hiyo lakini akamwomba amvumilie kidogo atoe salamu maalumu ya wana Mwanza.
Kama kawaida ya CHADEMA kwenye salamu yao, Wenje aliwaomba wananchi wakunje ngumi kisha akawasalimu kwa kibwagizo cha peoples… nao wakamwitikia power!
Akiwa katika viwanja vya Furahisha ambapo Rais Kikwete alichelewa kuanza mkutano wake, Wenje alifika hapo na kushangiliwa kwa nguvu na wananchi huku polisi wakiwazuia bila mafanikio.
Ilipofika saa 12 jioni kabla Rais hajaingia uwanjani, wananchi hao walimtaka Wenje awahutubie huku wakidai bendera ya taifa ishushwe kwani muda wake ulikuwa umefika.
Kikwete aliingia uwanjani hapo saa 12:10 akiongozana na viongozi mbalimbali wa chama na serikali lakini wananchi hawakuonyesha kumshangilia badala yake walikuwa wakimwonyesha alama ya vidole viwili inayotumiwa na CHADEMA wakiimba ‘peoples…power’.
Katika hatua ya kushangaza wananchi hao walimshangilia kwa nguvu mbunge wa Ilemela, Highness Kiwia, aliyekuwa ameongozana na Rais huku wakiwazomea Meya wa Manispaa ya Ilemela, Henry Matata, ambaye hakufika kabisa mkutanoni hapo.
Matata alionekana mapema wakati Rais Kikwete akisomewa taarifa ya maendeleo makao makuu ya wilaya hiyo lakini hakufika uwanjani kabisa katika viti vya mbele alionekana naibu wake, Swila Dede.
Baadhi ya wananchi hao walisikika wakisema chini kwa chini kuwa Matata ni mwizi hawataki kumsikia lakini shangwe na nderemo zikajiri pale walipotambulishwa Wenje na Kiwia.
Rais Kikwete akiwa wilaya ya Ilemela, wananchi wengi waliokuwa wamesimama njiani walimwonyesha vidole viwili ikiwa ni alama CHADEMA.
Hata hivyo, hali hiyo ilionekana kumkera kiongozi huyo wa nchi pamoja na maofisa wa usalama, ambapo wana usalama wakiwemo polisi walionekana wakiwatisha na kuwazuia wananchi kunyoosha vidole viwili.
Magufuli azomewa
Waziri wa Ujenzi, Dk. Magufuli, alikumbana na jinamizi la kuzomewa mbele ya Rais baada ya kusimama jukwaani na kutaja jina la Matata, ambapo wananchi wengi walimzomea kwa miluzi huku wakimnyooshea vidole viwili.
Adha Magufuli alizomewa pia aliposema wabunge wa Ilemela na Nyamagana jijini hapa ni wana CHADEMA lakini ndani ya roho zao ni wana CCM.
Pia aliendelea kuzomewa aliposema kuwa iwapo Rais angehitaji kupokea kadi za CHADEMA zilizorudishwa angepokea nyingi.
“Mheshimiwa Rais, nampongeza Meya Matata (akazomewa), lakini pia wabunge wa Ilemela na Nyamagana wanachapa kazi vizuri, nje CHADEMA lakini ndani wao CCM (akazomewa).”
Akizungumza katika mkutano huo, Rais Kikwete alimpongeza mbunge wa Nyamagana kwa uchapakazi mzuri hasa kusimamia sekta ya elimu na kwamba wabunge wa namna hiyo wanastahili kuigwa.
Hata hivyo, alisema serikali yake imejipanga vizuri kuhakikisha usafiri wa reli, ndege, majini na barabara za lami vinaboreshwa maradufu kwa ajili ya maendeleo ya wananchi.
“Serikali yangu imeweka nguvu kubwa katika kuboresha sekta ya uchukuzi, ujenzi na nyinginezo. Hii ni kutaka kuwaletea wananchi wetu maendeleo ya kisekta,” alisema.
Baadhi ya mawaziri walioongozana na Rais mbali na Magufuli ni Naibu Waziri, Ofisi ya Makamu wa Rais, Charles Kitwanga, Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Christopher Chiza, Waziri wa Maji, Prof. Jumanne Maghembe, Naibu Waziri wa Ujenzi na Dk. Charles Tizeba.

CANDIDATES TO BE SPONSORED BY MINISTRY OF HEALTH 2013/2014.

Friday, September 6, 2013

2014 Commonwealth Scholarships for Developing Commonwealth Countries’ Students in UK.

UK Department for International Development (DFID) offers Commonwealth Scholarships for developing countries’ students for pursuing Master’s, PhD and split-site (PhD) degree level at UK Universities. Approximately 300 scholarships are awarded each year. The CSC invites around three times more nominations than scholarships available – therefore, nominated candidates are not guaranteed to get a scholarship. There are no quotas for scholarships for any individual country. The application deadline for these Commonwealth Scholarships is 3rd December 2013.
Study Subject(s): Scholarships are provided in all subject areas offered at UK universities, although the CSC’s selection criteria give priority to applications that demonstrate strong relevance to development.
Course Level: Scholarships are available for pursuing Master’s, PhD, and split-site (PhD) degree level at UK Universities.
Scholarship Provider: UK Department for International Development (DFID)
Scholarship can be taken at: UK
Eligibility: To apply for the awards covered in this prospectus, candidates should:
-Be Commonwealth citizens, refugees, or British protected persons
-Be permanent resident in a developing Commonwealth country (a full list is available at http://bit.ly/cscuk-developing-cw-countries)
-Be available to commence their academic studies in the United Kingdom by the start of the UK academic year in September/October 2014
-Hold, by October 2014, a first degree of upper second class Honours standard (or above); or a second class degree and a relevant postgraduate qualification, which will normally be a Master’s degree and
-For awards enhance clinical skills in the fields of medicine and dentistry, have qualified as a doctor or dentist between 1 October 2004 and 30 September 2009.
-The Commission wishes to promote equal opportunity, gender equity and cultural exchange. Applications are encouraged from a diverse range of candidates.

HIVI NDIVYO MH.MBOWE ALIVYOONDOLEWA BUNGENI JANA.

UKUMBI wa Bunge leo uligeuka kuwa ulingo wa ngumi baada ya wabunge wa kambi ya upinzani kutunishiana misuri na askari wa bunge hilo ambapo  Kiongozi mkuu wa kambi ya upinzani Freeman Mbowe alipoamliwa kutoka nje na Naibu Spika Job Ndugai.

Hatua hiyo ilitokana  baada ya wabunge hao kupiga kura za kukubali au kukataa kuhusu kupitishwa kwa kujadili Mswaada wa Katiba uliopelekwa Bungeni hapo na Serikali ili kuweza kujadiliwa na bunge hilo.

Wabunge hao wa kambi ya upinzani wakiongozwa na Freeman Mbowe walipinga matokeo hayo na kuamua kusimama na wakati huo huo Spika Ndugai aliwataka kukaa chini ili kuendelea na kuchangia hoja za msingi za kujadili mswaada huo.

Ndugai aliwataka wabunge hao kukubaliana na matokeo yaliyotokea na kwa pamoja waweze kujadili mswaada huo 
ambao ni faida kwa taifa lakini mbali na ombi hilo kambi ya upinzani walikaidi ndipo Spika alitoa dakika tano kwa za kiongozi huyo kutoka ili bunge liendelee,ambapo hata hivyo kiongozi huyo alikaidi amri hiyo.

Baada ya mabishano hayo ndipo Spika alipotumia kiti chake na kuwataka askari wamtoe kwa nguvu nje ya ukumbi wa bunge, amri ambayo ilizua taflani na hekeheka kupelekea wabunge wa kambi ya wapinzani kuungana na kuwatunishia misuri askari hao wakimkingia kiongozi huyo kutolewa nje.

Tukio hilo lililochukua dakika zaidi ya 30 lilipelekea Bw. Job Ndugai kuwatolea macho askari hao akiwaamuru kutumia mabavu ili kuweza kumtoa nje ya ukumbi Bw. Mbowe.

Sakata hilo lilifanikiwa baada ya askari hao kutii amri ya Naibu Spika huo kwa kutumia mabavu kumtoa nje kiongozi wa kambi ya upinzani ambapo aliungwa mkono na wabunge  kutoka nje ya ukumbi na kususia kikao hicho.

Katika tukio hilo Mwenyekiti wa vyama vyenye wabunge wengi bungeni na Mbunge wa Jimbo la Vunjo Mkoani Kilimanjari Agustino Mrema alisema kuwa kitendo kilichofanywa na wabunge wezake si cha kungwa na na kinaleta fedheha kwa jamii na taifa kwa ujumla.

Alisema yeye kutokutoka kwake nje haimaanishi kuwa ni kibaraka wa CCM na  si ndicho alichotumwa kufanya na wananchi wake,hivyo haungi mkono hata kidogo na haeleweke hivyo kuhusu msimamo wake.

"Hatoki mtu hapa nitakaa ndani ya bunge mpaka kieleweke na mnielewe kwamba mimi ndiye kiongozi wao vyama vyote tisa,hivyo nastahili kuheshimiwa na sikubaki humu ndani kwa sababu mimi ni kibaraka wa CCM bali  kinachopiganiwa ni maslahi ya taifa na ndicho nilichotumwa na wananchi wangu sikutumwa nije kutoka nje au kususia bunge."alisema Mrema.

Naye, Mbunge wa Same Mashariki na Bi Anne Kilango Malecella aliitaka Serikali kusimama imara na isiogope vitisho vinavyotolewa na wasioitakiwa mema nchi katika kupigania maslahi ya taifa.

Alisema kuwa kitendo kilichofanywa na wapinzani bungeni hakina nia njema katika kupata katiba mpya na wajumbe 156 waliopiga kura wanavigenzo vya kuweza kuchangia Mswaada huo kujadiliwa.

Vurugu za bunge hilo ziliaza toka awali katika kipindi cha muongozo wa Spika ambapo vijembe,kashifa kwa wabunge kuzungumza bila kufuata utaratibu ilimradhimu Naibu Spika Job Ndugai kusimama mara kwa mara kujaribu kurejesha utulivu katika matukio yaliyotawala Ukumbini humo. 





Mara baada ya kutolewa mwongozo ulioombwa na wabunge juzi wakidai Muswada wa Mabadiliko ya rasimu ya katiba umeingizwa vipengele kinyemele, na Zanzibar kutoshirikishwa kikamilifu, wabunge wa kambi rasmi ya upinzani bungeni na wale wa CCM walikuwa wakituhumiana kusema uongo kuhusiana na hatua hiyo ya uandaaji wa mchakato wa Rasimu wa Katiba mpya.



Thursday, September 5, 2013

COMMONWEALTH SCHOLARSHIPS TENABLE IN THE UNITED KINGDOM FOR THE YEAR 2014.

The Ministry of Education and Vocational Training as a nominating agent in the country for the Commonwealth scholarships is inviting applications from qualified Tanzanians for Masters and Doctorate degrees tenable in the United Kingdom in the year 2014.

The Scholarships include:
·         One year taught masters courses or equivalent degrees.
·         Doctorate degrees, of up to three years duration.

Qualifications
1.    Applicants must be holders of bachelor or masters degrees;
2.    Applicants for masters must have bachelor degrees of GPA not less than 3.5; and
3.    Applicants for Doctorate degrees must have a B Grade Masters degrees or a GPA of 4.0 or above at Masters level.

Mode of Application:
·        All applications should be made directly to the Commonwealth Secretariat and should be online using the following link: http://bit.ly/cscuk-apply
·         It is important that applicants should read and understand all given instructions when filling the application forms, and should attach all necessary attachment such as certified copies of academic certificates, transcripts, birth certificates and submit online through the above mentioned link.

All applicants who wish to be nominated by the Ministry of Education and Vocational Training, should print one hard copy of completely filled application form, attach with certified photocopies of academic certificates, transcripts, and birth certificates and submit them to the address below before 15th October, 2013.


The Permanent Secretary,
Ministry of Education and Vocational Training,
P. O. Box 9121,
DAR ES SALAAM

KATIBU MKUU WA CCM TAIFA KUFANYA ZIARA KATIKA MIKOA YA SHINYANGA,MARA NA SIMIYU.



Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Ndugu Abdulrahaman Kinana septemba 10 anatarajiwa kuanza ziara ya kawaida katika mikoa ya Shinyanga, Simiyu na Mara.

Ziara hiyo itaanzia katika mkoa wa Shinyanga septemba 10 mpaka 13 mwaka huu, kwa kutembelea wilaya zote nne za mkoa huo na kufuatiwa na mkoa mpya wa Simiyu kuanzia Septemba 14 mpaka septemba 19 kwa kutembelea wilaya zote tano Kabla ya kuhitimisha ziara hiyo kwa kutembelea wilaya Sita za mkoa wa Mara kuanzia Septemba 20 Mpaka 25 mwaka huu.

Katika ziara hiyo Katibu Mkuu wa CCM ataambatana na Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM anayeshughulikia Itikadi na Uenezi Ndugu Nape Nnauye.

Kwa mujibu wa Ratiba ya ziara hiyo, Wajumbe hao wa sekretarieti watakagua uhai wa Chama ikiwa ni pamoja na kupokea wanachama wapya sanjari na kuhamasisha wananchi kujituma katika shughuli za uzalishaji ili Kuleta tija katika maisha Yao na ya taifa kwa ujumla.

Aidha watakagua maendeleo ya utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010/2015 hasa katika miradi ya kimaendeleo Kama vile Ujenzi wa majosho kwa ajili ya wafugaji, maendeleo ya maboresho ya kilimo cha Pamba, uvuvi wenye tija pamoja na maboresho ya sekta za Afya, elimu na miundombinu zikiwemo Barabara.

Katika ziara hiyo Katibu Mkuu  atapata fursa ya kusikiliza kero mbalimbali za wananchi na kwa kushauriana na serikali kutafuta namna ya kuzitafutia ufumbuzi.Katibu mkuu pia atafanya mikutano ya ndani, na ya hadhara katika kila wilaya za mikoa hiyo.
 

Imetolewa na;
Nape Moses Nnauye
Katibu wa Itikadi na Uenezi
05/09/2013

ALICHOKISEMA ZITTO KABWE JUU YA WAHAMIAJI HARAMU KUTOKA KIGOMA.

 
Watanzania kutoka mkoa wa Kigoma waliokamatwa jana huko Tegeta wameachiwa baada ya kuingilia kati. Tumepata taarifa kuwa kuna wengine kutoka maeneo ya Kitunda pia walikamatwa jana. Tunaendelea kufuatilia. Tutaweka hapa jina la kila aliyekamatwa, kijiji anachotoka na alikamatwaje.
Tunaunga mkono juhudi zozote za kuzuia wahamiaji haramu. Hata hivyo lazima zoezi hili liendeshwe kwa umakini mkubwa sana. Nchi yetu inapakana na nchi 8. Ni dhahiri kama kila mtu anayetoka mkoa wa pembezoni ni 'suspect' wa uraia, tutagombana sana. Ni vema vitambulisho vya Taifa vitoke haraka kwa watu wa mipakani ili kuondoa hizi 'harassment'

MAONI YA MSEMAJI WA KAMBI RASMI YA UPINZANI BUNGENI, WIZARA YA SHERIA NA KATIBA, MHESHIMIWA TUNDU A.M. LISSU KUHUSU MUSWADA WA SHERIA YA MAREKEBISHO YA SHERIA YA MABADILIKO YA KATIBA, YA MWAKA 2013

(Kanuni ya 86(6) ya Kanuni za Kudumu za Bunge, 2013)
UTANGULIZI
Mheshimiwa Spika,
Huu ni Muswada wa marekebisho ya pili ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, Sura ya 83 ya Sheria za Tanzania. Kama Bunge lako tukufu litakavyokumbuka, Sheria hii ilifanyiwa marekebisho ya kwanza kwa kupitishwa kwa Sheria ya Marekebisho ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, Na. 2 ya mwaka 2012, mwezi Februari ya mwaka jana. Mabadiliko hayo ya kwanza yalihusu Sehemu ya Tatu na ya Nne ya Sheria hii, na yalilenga vifungu mbali mbali vinavyohusu Tume ya Mabadiliko ya Katiba na utekelezaji wa majukumu yake.
Muswada huu wa sasa unalenga kufanya marekebisho katika Sehemu ya Tano ya Sheria inayohusu ‘Kuitisha Bunge Maalum.’ Sambamba na mapendekezo haya, kuna mapendekezo ya kufanya marekebisho katika Sehemu ya Sita kwa kufuta vifungu vya 32 hadi 36 vya Sheria vinavyohusu utaratibu wa kura ya maoni kwa ajili ya kuhalalisha ‘Katiba Inayopendekezwa.’ Marekebisho haya yamewekwa katika aya ya 57 ya Muswada wa Sheria ya Kura ya Maoni, 2013. Mapendekezo ya Muswada huu ni muhimu lakini yana utata mkubwa.
Mheshimiwa Spika,
Katika kutekeleza majukumu yake ya kuuchambua Muswada huu, Kamati ya Bunge lako tukufu ya Katiba, Sheria na Utawala ilikutana na wadau wengi mbali mbali. Hivyo, kwa mfano, Kamati ilipata maoni ya taasisi za kidini na za kiraia; taasisi za elimu ya juu na za kitaaluma; vyama vya siasa na asasi nyingine. Kwa sababu ambazo Kamati haikuelezwa vizuri na uongozi wa Bunge hili tukufu, mapendekezo ya Kamati kwenda Zanzibar kwa lengo la kukusanya maoni ya wadau wa Zanzibar juu ya Muswada huu muhimu kwa mustakbala wa Jamhuri ya Muungano yalikataliwa.
Kwa maana hiyo, ni muhimu Bunge lako tukufu lifahamu ukweli huu kwamba wadau pekee walioshirikishwa kutoa maoni yao juu ya Muswada ni Watanzania Bara tu. Wazanzibari hawakupatiwa fursa hiyo na hawakushirikishwa kabisa, licha ya Sheria yenyewe kuwa na mambo mengi yanayoihusu Zanzibar. Kwa vile wadau wa Zanzibar walishirikishwa kikamilifu kutoa maoni yao kuhusu Muswada uliopelekea Sheria hii kutungwa mwaka 2011, Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni inataka kujua ni kwa nini uongozi wa Bunge na wa Serikali umeona si busara na sahihi kuwapatia Wazanzibari fursa ya kutoa maoni yao kuhusu Muswada huu wa kurekebisha Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ambayo inawahusu pia Wazanzibari na nchi yao.
URAIS WA KIFALME KWA MARA NYINGINE TENA!!!!
Mheshimiwa Spika,
Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni imepigia kelele jitihada za serikali hii ya CCM kudhibiti mchakato wa Katiba Mpya kwa kuendeleza kile tulichokiita miaka miwili iliyopita, “... kivuli kirefu cha Urais wa Kifalme katika mchakato wa upatikanaji wa Katiba Mpya.[i] Hapo tulikuwa tunazungumzia mamlaka ya Rais ya uteuzi wa Wajumbe na watendaji wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, na tulisema kwamba mamlaka hayo yalikuwa na lengo moja tu: “kuhakikisha kwamba matokeo ya kazi ya Tume hiyo ni yale tu yanayotakiwa na Rais na Serikali yake na chama chake cha CCM.
Mheshimiwa Spika,
Katika Maoni yetu wakati wa kutungwa kwa Sheria hii mwezi Novemba mwaka 2011, Kambi Rasmi ya Upinzani ilipinga vikali mapendekezo ya kumwezesha Rais kuteua Wajumbe wa Bunge Maalum wasiotokana na Bunge lako tukufu na Baraza la Wawakilishi Zanzibar. Tulisema yafuatayo kuhusiana na jambo hili: “... wajumbe ... wanaopendekezwa kuteuliwa kwenye Bunge la Katiba kwa mujibu wa ibara ya 20(2)(e) na (4) ya Muswada Mpya sio, na hawawezi kuwa, wawakilishi wa wananchi. Kwanza, hawajachaguliwa na mtu yeyote na wala taasisi zao kuwawakilisha katika Bunge la Katiba kwa sababu Muswada Mpya unapendekeza wateuliwe na Rais.
Kwa sababu ya upinzani huo, mapendekezo ya kumfanya Rais kuwa mteuzi wa wajumbe wa Bunge Maalum wasiokuwa wabunge na Wawakilishi yaliondolewa katika Muswada huo wa Sheria hii. Badala yake, kifungu cha 22(1)(c) cha Sheria iliyotungwa na Bunge lako tukufu kiliweka wazi kwamba “wajumbe mia moja sitini na sita [watateuliwa] kutoka ...” taasisi zilizotajwa katika kifungu hicho.
Mheshimiwa Spika,
Ni kweli kwamba kifungu cha 22(1)(c) kama kilivyotungwa kilileta giza badala ya mwanga katika suala la uteuzi wa wajumbe hao. Kama tulivyoieleza timu ya wataalamu wa Serikali kufuatia mkutano wetu na Rais Jakaya Kikwete uliofanyika Ikulu tarehe 26 Novemba, 2011: “Toleo la Kiswahili la Sheria linasema kwamba wawakilishi wa makundi mengine ‘watakaoteuliwa kutoka’ kwenye makundi yaliyoorodheshwa. Toleo la Kiingereza linasema wajumbe hao watakuwa ‘drawn from’ (kwa tafsiri ya Kiswahili ‘watachukuliwa kutoka’). Maana za maneno haya hazifanani na wala hayako wazi kuhusu nani ‘atakayewateua’ au ‘kuwachukua’ wajumbe hao kutoka kwenye taasisi zao.[ii]
Kwingineko katika mkutano wetu na Rais Kikwete tulimweleza kwamba: “Wajumbe 166 wengine wanaowakilisha taasisi nje ya Wabunge na Wawakilishi hawajachaguliwa na mtu yeyote na wala na taasisi zao kwani Sheria haisemi ni nani atakayewateua na/au kuwachagua.” Kwa sababu hiyo, tulipendekeza kwamba “Sheria iweke wazi kwamba wajumbe hawa ‘watateuliwa na’ taasisi zilizotajwa. Hii itaondoa utata juu ya uwakilishi wao na juu ya mamlaka yao ya uteuzi.[iii]


LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...