Saturday, June 29, 2013

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI KUKANUSHA BAADHI YA MATANGAZO KATIKA MITANDAO YA KIJAMII.

Katibu wa Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma Bw. Xavier Daudi wakati akizungumza na wandishi wa Habari Ofisini kwake kuhusu maswala mbalimbali ya Ofisi yake. Kulia kwake ni Naibu Katibu Idara ya Ajira Bw. Lucas Mrumapili.

 

Taarifa ya Kukanusha Baadhi ya Matangazo katika Mitandao ya Kijamii

Ndugu Wandishi wa Habari, kwanza niwashukuru kwa kuitikia wito, nimewaita hapa kwa mambo mawili.
Awali ya yote nianze kwa kuwapongeza kwa kazi nzuri mnayoifanya katika kuelimisha umma  juu ya masuala mbalimbali yakiwemo ya kiuchumi, kisiasa na kijamii licha ya changamoto mbalimbali mnazokumbana nazo katika utekelezaji wa majukumu yenu.

Baada ya kusema hayo, nianze kueleza nilichowaitia hapa nikitambua umuhimu  wa nafasi yenu katika jamii hususan katika kuelimisha umma kupitia vyombo vyenu.   Moja ya kazi za msingi za taasisi yetu kwa mujibu wa sheria iliyoanzisha Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma ni kutangaza nafasi wazi za Ajira kwa mujibu wa mahitaji.

Napenda kutoa rai kupitia  kwenu na kwa wadau wetu wote watambue kuwa ni kosa kwa mtu au taasisi yoyote kuchukua matangazo ya Sekretarieti ya Ajira bila idhini na kuyafanyia marekebisho.  Vile vile ni kosa kwa mujibu wa sheria kuandaa  matangazo mbalimbali yanayohusiana na Mchakato wa Ajira katika Utumishi wa Umma kwa lengo la kupotosha umma ilhali wakijua wazi kuwa taarifa hizo wanazozichapisha au kuziandika katika baadhi ya mitandao ya kijamii siyo halali na hazijatolewa na Sekretarieti ya Ajira.

TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UTUMISHI, JULAI 2013.

HIVI NDIVYO SUGU ALIVYOACHILIWA HURU KATIKA KESI YAKE VS WAZIRI MKUU.

MWENDESHA Mashitaka wa Serikali (DPP) jana asubuhi aliambulia patupu baada ya Hakimu wa Mahamaka ya Hakimu Mkazi wa Wilaya ya Dodoma, kumwachia huru Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi, (CHADEMA) ambaye alimfikisha kizimbani kujibu tuhuma za kumkashifu Waziri Mkuu, Mizengo Pinda kupitia mitandao ya kijamii.

Wakili wa Mbilinyi ambaye ni Mwanasheria na Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (Mb, CHADEMA), aliitaka mahakama ifutilie mbali shitaka alilofunguliwa mteja wake kwa kudai kuwa halina msingi wowote wa kisheria.Baada ya mabishano ya kisheria baina ya Lissu na Mwanasheria wa Serikali kushindwa kuthibitisha kuwa neno, “mpumbavu” ni lugha ya matusi,
ndipo Hakimu alipoamua kulifuta shitaka lililowasilishwa kwake na kumwambia DPP akatengeneze upya mashitaka yake kwani aliyoyapeleka yalikuwa na hitilafu kubwa.

Naye Lissu ametaka kesi mpya itakayoletwa mahakamani iwe na maelezo ya Waziri Mkuu na awe tayari kusimama mahakamani kuthibitisha shitaka hilo.

Kesi hiyo ilikuwa ikisikilizwa na Hakimu Mkazi Mfawidhi, Elinaza Luvanda.

Awali akimsomea mashtaka, Mwendesha Mashtaka wa Serikali, Harriet Lopa alidai kuwa Juni 24, mwaka huu, Mbilinyi akiwa Dodoma alituma ujumbe wenye lugha ya matusi kwa kutumia mtandao wa kijamii wa Facebook kwa Waziri Mkuu Mizengo Pinda.

Mshtakiwa alikana shitaka hilo na Wakili wa Mshtakiwa, Lissu aliomba kutoa hoja na kusema hati ya mashtaka ni mbovu na kuomba Mahakama itupilie mbali kwa sababu ina makosa.

“Lugha ya matusi haikutajwa, lugha gani hiyo ya matusi na hati ya mashtaka iko kimya, mshtakiwa atajitetea vipi,ataandaa utetezi namna gani kwani hata kinachodaiwa kuwekwa kwenye facebook hakijasemwa,” alidai Lissu.

Akijibu hoja hiyo, Wakili wa Serikali alisema kesi hiyo bado iko kwenye upelelezi na kutaka mshtakiwa aendelee na mashtaka yake mpaka itakapothibitishwa vinginevyo.

Kutokana na kauli hiyo ya wakili wa Serikali, Lissu alizidi kusisitiza hati ya mashtaka haina maelezo ya kutosha na inatakiwa kukidhi matakwa ya sheria.

“Hati ya mashtaka iliyoletwa si halali kinyume na kifungu cha 132 cha mwenendo wa makosa ya jinai na itakuwa makosa kama Mahakama ikikubali hati hiyo,” alisema.

Alitoa uamuzi wa Mahakama, Hakimu Luvanda alisema anakubaliana na maelezo ya Wakili upande wa utetezi Lissu kuwa hati hiyo ina mapungufu.

Alisema Mahakama inamuachia huru mshtakiwa na upande wa mashtaka unaweza kumshtaki tena mshtakiwa kama itaona umuhimu wa kufanya hivyo.

Akizungumza nje ya Mahakama Lissu alisema hati ya mashtaka dhidi ya Mbilinyi kuwa alitoa lugha ya matusi kwa Waziri Mkuu Mizengo Pinda haijaeleza anachodaiwa kusema Mbilinyi.

Alisema Mahakama imetenda sawasawa kuifuta hati hiyo ilitakiwa ifafanue lugha ya matusi iliyotumika ni ipi. ”Hakimu hajasema Sugu hana makosa, lakini upande wa mashtaka ukajipange kutengeneza hati mpya,” alisema.

WACHEZAJI 2 WACHAGULIWA KITUO CHA VIPAJI ASPIRE


Wachezaji wawili kutoka Tanzania wamechaguliwa miongoni mwa 50 waliofanyiwa majaribio nchini Uganda kwa ajili ya kuingia katika kituo cha kuendeleza vipaji (centre of excellence) kilichoko Doha nchini Qatar kupitia mpango wa kukuza vipaji wa Aspire Football Dream.
Abdulrasul Tahir Bitebo (15) ambaye ni mshambuliaji kutoka Kituo cha Uwanja wa Karume, na Martin Omela Tangazi (14) ambaye ni beki kutoka Kituo cha Ukonga ndiyo waliochaguliwa kutoka Tanzania kuingia katika kituo ambapo watakaa kwa mwezi mmoja kabla ya kusaini mkataba rasmi wa kuendelezwa.
Wachezaji wengine walikuwa wakitoka katika nchi za Uganda na Kenya. Mchezaji mwingine aliyefuzu katika nafasi tatu zilizokuwepo ni kutoka nchini Kenya.
Mpango wa Aspire Football Dream unafadhiliwa na Mtoto wa Mfalme wa Qatar katika nchi 16 duniani, na kwa hapa nchini uko chini ya Idara ya Ufundi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF).
TFF ina jumla ya vituo 14 vya kuendeleza vipaji kupitia mpango huo wa Aspire Football Dream. Vituo hivyo ni Karume, Kigamboni, Tandika, Kawe, Ukonga, Kitunda, Mbagala, Magomeni, Makongo, na Tabata vilivyo katika Mkoa wa Dar es Salaam. Vingine ni Bagamoyo kilichopo mkoani Pwani, Morogoro, Arusha na Moshi mkoani Kilimanjaro.
Kituo kingine cha kuendeleza vipaji (centre of excellence) cha Aspire kipo Dakar nchini Senegal.

TFF KUENDESHA KOZI 6 KATI JULAI NA SEPTEMBA 2013

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) litaendesha kozi sita tofauti za mpira wa miguu kati ya Julai na Septemba mwaka huu.
Kozi hizo ni FIFA 11 For Health itakayofanyika Hombolo mkoani Dodoma kuanzia Julai 8 hadi 19 mwaka huu. Julai 6 hadi 15 mwaka huu kutakuwa na kozi ya mpira wa miguu wa ufukweni (Beach Soccer) itakayofanyika jijini Dar es Salaam.
Waamuzi wa FIFA nao watakuwa na kozi itakayofanyika kati ya Agosti 22 hadi 26 mwaka huu jijini Dar es Salaam wakati kozi ya ukocha kwa ajili ya Copa Coca-Cola itafanyika jijini Dar es Salaam kati ya Agosti 12 na 17 mwaka huu.
Vilevile kutakuwa na kozi ya mpango wa grassroots unaolenga wachezaji mpira wa miguu (wasichana na wavulana) wenye umri kuanzia miaka 6-12 itafanyika kuanzia Septemba 9 hadi 13 mwaka huu jijini Dar es Salaam wakati tamasha (festival) la grassroots litafanyika Uwanja wa Karume, Septemba 14 mwaka huu.

Scholarships for Undergraduates in Canada 2014.

University of British Columbia offers International Leader of Tomorrow Award for undergraduates in Canada. To be considered for the  award, students must be admissible to the first choice program they are applying to, including meeting UBC’s English Language Admission Standard. Applicant should be an international student, who is neither a Canadian citizen nor a permanent resident of Canada, and who will be studying in Canada on a Canadian Study Permit (visa). Award-winners receive an award-level commensurate with their financial need as determined by the costs of their tuition, fees and living costs. The deadline for nomination packages to be received at UBC is December 10, 2013.
Study Subject(s): Scholarships are provided to learn any of the courses offered by the University of British Columbia.
Course Level: Scholarships are available for pursuing undergraduate degree level at University of British Columbia.
Scholarship Provider: University of British Columbia
Scholarship can be taken at: Canada

TANAPA NEW TARIFFS VALID FROM JULY 1st, 2013 TO JUNE 30th, 2015

MAELEZO YA WAKILI KIBATARA JUU YA TUHUMA ZA KIONGOZI WA CHADEMA DAR HENRY J. KILEO.


BAADA ya sintofahamu kuhusu kilichomsibu kiongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA Mkoa wa Dar es Salaam, Henry John Kileo, utata wa Jeshi la Polisi na juhudi za mkewe Joyce Kiria kutaka kujua aliko mumewe, nimeona nitoe kile kilichotokea katika sakata hili.
Kileo alipigiwa simu na maofisa wa polisi makao makuu mnamo tarehe 17/6/2013, wakimuarifu kwamba wanataka kufanya mahojiano naye. Hawakusema ni kuhusu nini.
Mara moja akawasiliana nami kama wakili wa familia yao, nami nikawasiliana na maofisa hao kuwaarifu kwamba kwa kuwa nina majukumu kadhaa ya kimahakama, na kwa kuwa Kileo yuko nje ya mkoa, basi ninaahidi kama wakili kuhakikisha nitampeleka binafsi Makao Makuu Polisi Ijumaa ya tarehe 21/6/2013.
Tarehe 21/6/2013 tuliambatana mimi, Kileo na John Mnyika (MB) hadi Polisi Makao Makuu, kisha Mnyika alituacha na mahojiano yakaanza.
Kwa ujumla walimuhoji Kileo mambo mbalimbali kuhusiana na tukio la kumwagiwa tindikali kijana aitwaye Mussa Tesha katika uchaguzi mdogo wa Jimbo la Igunga mnamo mwaka 2011.
Wakati mahojiano hayo yanafanyika, tayari kulikuwa na kesi ya jinai ikiendelea huko Igunga, mkoani Tabora ambako washitakiwa wanne ambao ni makada wa CHADEMA kutoka maeneo mbalimbali nchini walishitakiwa kama mshtakiwa nambari moja mpaka nne kuhusiana na tukio hilo la Tesha. Walishitakiwa chini ya vifungu vya sheria ya kanuni ya adhabu (Penal Code), na si ugaidi.
Baada ya mahojiano yaliyomalizika kwa Kileo kuandikisha maelezo hadi mnamo saa 11.30 hivi za jioni, polisi walimnyima dhamana, na wakampeleka rumande iliyoko Kituo Kikuu cha Polisi (Central Police Station), akalala huko.
Jumamosi ya tarehe 22/6/2013, mimi Joyce na Mnyika tulifika Kituo Kikuu cha Polisi, ambapo OCS wa hapo alituarifu kwamba amri alizonazo ni kwamba Kileo haruhusiwi kuonana na mtu yeyote.
Kama wakili, nilijadiliana masuala ya kisheria na OCS, ikalazimu kuwasiliana na maofisa wa polisi makao makuu ambao hatimaye waliniruhusu kwa mujibu wa sheria kuonana na mteja wangu.


Friday, June 28, 2013

"KILI MUSIC TOUR" SASA KUWASHA MOTO MKWAKWANI TANGA.

Tanzania Breweries Limited (TBL) chini ya kinywaji chake cha Kilimanjaro,  inaendelea na ziara ya tamasha kubwa la muziki la ‘Kili Music Tour 2013’ ambapo wikiendi hii ya Jumamosi ya tarehe 29 mwezi Juni,  litafanyika Mjini Tanga kwenye kiwanja cha Mkwakwani likijumuisha wasanii wakali wanane ambao ni Ally Kiba, Snura Mushi, Professor J, Mwana FA, Recho, Mzee Yusuph, Roma na Kala Jeremiah.
Ziara ya Kili Music Tour ilianzia Dodoma wiki iliyopita na kuacha kumbukumbu isiyofutika kwa wakazi wa Dodoma na viunga vyake, ambao walipata burudani kutoka kwa wasanii nyota kama vile Ben Pol, Roma, Ally Kiba, Linex, Professa Jay, Ommy Dimpoz, Lady Jay Dee pamoja na Mkali Kala Jeremiah.

Kili Tour kwa mwaka huu inakujia ikiwa na kauli mbiu ya “Kikwetu kwetu” kwani burudani itayokuwa ikitolewa ni kutoka kwa wasanii wa nyumbani, wakikupa ladha za ala za muziki wa nyumbani na katika viwanja vya nyumbani.

Kama kawaida, mambo yataanza saa 10 jioni, jumamosi hii pale Mkwakwani na unakabidhi shilingi elfu mbili na mia tano mlangoni, ambapo utapata bia moja bureee, unaingia unapata burudani kutoka kwa wasanii bora kabisa Tanzania, Kili Music Tour 2013, Kikwetu Kwetu zaidi.

OBAMA KUTUNUKIWA PhD NA THE OPEN UNIVERSITY OF TANZANIA.


UJIO WA OBAMA,NDEGE 8 ZA KIJESHI NA MELI ZTUA DAR KUIMARISHA ULINZI.

Makachero wa Marekani wameendelea na matayarisho ya mwisho ya ziara ya Rais Barack Obama, ambapo katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere walikuwa na kazi ya kuunganisha helikopta za doria.
Makachero hao walikuwa wakiunganisha helikopta sita zilizosafirishwa vipande vipande kutoka Marekani, ambapo meli mbili za kivita na ndege moja pia zimewasili.
Rais Obama tayari yuko katika ardhi ya Afrika, ambapo leo anatarajiwa kwenda Afrika Kusini baada ya kumaliza ziara yake ya kwanza Senegal na anatarajiwa kuwasili nchini Jumatatu.
Kwa mujibu wa uchunguzi uliofanywa jana na Mwananchi unaonyesha Marekani imeleta helikopta hizo kwa ajili ya ulinzi wa Rais Obama, zikiwemo meli zilizobeba helikopta nyingine mbili na ndege.
Habari zilizopatikana kutoka kwa wafanyakazi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere,zinasema kuwa helikopta sita zinaunganishwa katika sehemu ya karakana ya Kikosi cha Anga cha Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).
Mpashaji mmoja aliliambia gazeti hili kuwa helikopta hizo zililetwa kama vipande vipande vilivyosafirishwa kama mzigo kwenye meli za kivita zilizotia nanga jijini Dar es Salaam.
“Nilikaribia kwenye eneo la karakana na nikashangaa kuona jinsi jamaa walivyokuwa ‘bize’ wakiunganisha vyuma mbalimbali na kutengeneza helikopta hizo,” aliongeza mpashaji wetu, ambaye alibahatika kusogelea eneo hilo licha ya kuwepo kwa ulinzi mkali.
Inaaminika kuwa helikopta hizo zitakuwa zinasaidia kusafirisha watu na mizigo kutoka kwenye meli za kivita ambazo zimeegeshwa kwenye Kikosi cha Maji cha JWTZ.
Pia helikopta mbili zinaaminika ziko katika meli ambazo zimeegeshwa huko Kigamboni.


TANGAZO KWA WALIOPANGIWA VITUO VYA KAZI AFYA WAKIWA KWENYE MAFUNZO KWA VITENDO (INTERNSHIP).

Thursday, June 27, 2013

ACCESS COURSE JOINING FORM - RWEGALURILA.

CANDIDATES SELECTED TO JOIN ACCESS COURSE- RWEGALURILA.

WAFANYABIASHARA WAGOMA UGANDA KWA SIKU 3 SASA.

Maduka yamesalia kufungwa mjini Kampala Ugana kwa siku ya tatu leo huku wafnyabiashara wakigoma kuhusiana na mpango wa serikali kusisitiza viwango vya biadhaa zinazoingizwa nchini humo kuwa za juu.

Chama cha wafanyabiashara hao kinasema kinapinga gharama wanayotozwa ikiwa bidhaa wanazoingiza nchini humo sio za viwango vya juu. Malipo hayo ni kodi iliyoanza kutozwa na serikali hivi karibuni ambayo inagharamia kuchunguzwa kwa bidhaa zinazoingizwa nchini humo
Wanatak serikali ikome kuwatoza ushuru huo kwani wafnyabiashara tayari wanatozwa kodi ya juu.
Duru zinasema kuwa vuguvugu la upinzani linatarajiwa kujiunga na maandamano hayo, na kuwa polisi wamedhibiti hali ya usalama mjini Kampala.
Mwandishi wa BBC mjini humo Catherine Byaruhanga anasema kuwa polisi huenda wakavunja maandamano hayo kwa kuhofia otovu wa usalama.
Waziri wa biashara, Amelia Kyambadde, ameelezea wazi kuwa Uganda inashinikizwa na wanachama wa jumuiya ya Afrika Mashariki kuwa iweze kutekeleza vikwazo vya kuhakikisha kuwa bidhaa zinzoingizwa nchini humo ziwe za hali ya juu.
Kodi hiyo inalenga kuondoa uwezekano wa wafanyabiashara kuingiza biadhaa ghushi nchi humo swala ambalo Uganda inatuhumiwa kutokuwa maakini nalo katika kulitokomeza.
Wafanyabiashara wanapaswa kuingiza nchini humo bidhaa za hali ya juu kutoka kwa watengezaji wanaojulikana na ambao wako kwenye orodha inayojulikana kwa mataifa ya Afrika Mashariki, ingawa wanasema kuwa gharama inayopaswa kulipwa kwa hilo kufanyika ni ya juu zaidi.

Source:BBC

JACOB ZUMA AHAIRISHA SAFARI YA MSUMBIJI BAADA YA HALI YA MANDELA KUZIDI KUZOROTA.


Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma amefutilia mbali ziara yake ya kwenda Musumbiji baada ya kumtembelea hospitalini aliyekuwa Rais wa Afrika Kusini, Nelson Mandela. Rais Zuma amesema kuwa Bwana Mandela yuko katika hali mbali ya afya.
Msemaji wa Zuma Mac Maharaj amesema kuwa hali yake imedorora zaidi katika saa 48 zilizopita.
Mandela ambaye, ni Rais wa kwanza mweusi wa Afrika Kusini, amelazwa hospitalini tangu tarehe 8 mwezi Juni akiugua maradhi ya mapafu.

University of Abertay Dundee Overseas Student Scholarships in UK, 2013/14.

University of Abertay Dundee is funding International Scholarships for students living outside the European Union and the European Free Trade Area and who are liable to pay overseas tuition fees. Various Academic Merit and Personal Achievement Scholarships are offered. The Overseas Student Scholarship Fund will support individual scholarships based on academic merit, and/or personal achievement in either sports or music. Scholarship is available for international students living outside the EU and enrolled for undergraduate and postgraduate study at Abertay for September 2013. Students may apply multiple scholarships but only one scholarship is awarded. Scholarship deadline is 31st July 2013.
Study Subject(s): Scholarships are provided to learn any of the courses offered by the University of Abertay Dundee in UK.
Course Level: Scholarships are for pursuing undergraduate and postgraduate degree at University of Abertay Dundee in UK.
Scholarship Provider: University of Abertay Dundee
Scholarship can be taken at: UK

KUJA KWA OBAMA, MEMBE AZUIA SAFARI ZA DAR KWA SIKU 10.

Waziri wa Mambo ya Nje, Bernard Membe amewashauri watu walioko mikoani kusitisha safari za kuja Dar es Salaam wakati wa ziara ya Rais wa Marekani, Barrack Obama kutokana na wingi wa wageni katika jiji hilo.
Ugeni huo pamoja na ule wa viongozi kumi na moja kutoka nchi mbalimbali duniani watakaohudhuria mkutano wa kimataifa wa Smart Partnership utakaofunguliwa kesho na Rais Jakaya Kikwete kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere, umesababisha kuimarishwa kwa ulinzi katika maeneo mbalimbali hasa katika hoteli za kitalii ambazo zimeanza utaratibu wa upekuzi kwa wageni wake.
Akizungumza katika mahojiano na Redio ya Clouds jana, Membe alisema jiji limefurika kwa wingi wa wageni.
“Hoteli na nyumba za wageni zimefurika wageni na magari mengi yamekodiwa. Kwa ujumla, huduma za kijamii zitakuwa shida,” alisema.
Rais Obama na mkewe Michelle watawasili nchini Jumatatu na tayari wapambe na maofisa usalama kutokana Marekani wameanza kuwasili. Mbali ya ujio huo, wake wa marais kutoka nchi 14 za Afrika watakaokutana na Laura Bush, mke wa Rais wa zamani wa Marekani, George Bush. Pia Michelle atahudhuria mkutano huo utakaofanyika Jumanne na Jumatano ijayo.
“Jiji la Dar es Salaam litakuwa na mambo mengi kwa hiyo wale wenye kuja kutaka kustarehe wafute safari zao,” alisema na kuongeza: “Kama kuna watu ambao hawapo Dar es Salaam na hawana sababu za kuja mjini waache tu mpaka wageni watakapoondoka kwa sababu jiji la litakuwa limejaa na baadhi ya barabara zitachukuliwa zitumike na wageni hao.”
Alisema katika kipindi cha siku tano zijazo, baadhi ya barabara za Jiji la Dar es Salaam zitakuwa na shughuli nyingi na nyingine zitalazimika kufungwa. Barabara itakayofungwa ni pamoja na ile ya Mwai Kibaki na ile ya Bagamoyo itakuwa na shughuli nyingi pia wakati Michelle atakapokwenda Jumba la Makumbusho, Jumanne ijayo.
Wasafiri wa mikoani.

HII NDO KAULI YA KAMANDA WILFRED LWAKATARE

Na Wilfred Lwakatare,
Sina budi kumshukuru sana mwenyenzi Mungu kwa kunitendea mema na zaidi ya yote kunipa uhai na afya hadi sasa. Wanasema “shukuruni katika yote” na mimi nalazimika kushukuru kwa yale yote niliyofunuliwa na kuwa sehemu ya ushuhuda wangu katika maisha niliyobakiza hapa duniani.

Namshukuru Mungu muweza wa yote kwa kunirejesha tena uraiani na kwa kuniunganisha na familia yangu,mke na watoto,wazazi ,ndugu,majirani na marafiki,viongozi wenzangu na wanachama wa chama kikubwa CHADEMA na zaidi ya yote watanzania walio wazalendo wanaoipenda na kuipigania nchi yao.

Ninapojikuta huru nje ya milango ya mninga uliowekewa makufuli makubwa,madirisha yenye nondo,ukuta uliowekewa waya wenye miiba mikali na ulinzi wa maaskari wanaonichunga saa 24,inanikumbusha wimbo mmoja wa mchakamchaka uliokuwa ukiimbwa gerezani kila siku saa 11:00 alfajiri tunapoamshwa uliokuwa na maneno;

“Kama raia!kama raia!kama raia!kama raia!
Iko siku moja nitarudi kwetu kwa baba na mama kama raia!
Iko siku moja nitarudi kwetu kwa ndugu na rafiki kama raia!
Kama raia…….”

Ni kweli kabisa na wala si hadithi kuwa ‘jela ni MBAYA, jela ni MATESO!’ Lakini zaidi ya hilo, kwangu mimi nimeyaona pia maisha ya gerezani ni mahala pa mafunzo ya kuijua jamii, kuyajua maisha, kuyaelewa mambo, kuifahamu nchi n.k.

Nimekubaliana mia kwa mia na maneno ya mwenyekiti wetu wa CHADEMA-Taifa Freeman Mbowe(MB) aliponitembelea gerezani Segerea na kuniambia; “hupaswi kulia na kujuta sana;now you are going to be a PRISON GRADUATE, uhitimu ambao kila mwanasiasa na mpigania haki mahiri duniani ameupitia.” Kipindi cha siku 92 nilichokaa ndani nikianzia polisi kituo cha kati, gereza la Keko na kisha kumalizia Segerea kimenipa uzoefu na ufahamu usio wa kawaida.

Ipo tofauti kubwa baina ya idara za polisi na magereza,jambo ambalo lilikuwa nje ya ufahamu wangu kabla.Nina uhakika magereza wakipewa kazi ya kuwasaka walipua mabomu ,watesaji,wapiga risasi mapadri watawakamata. Nilipata bahati ya kuitwa na kufanya mazungumzo na wakuu wa magereza ya Keko na Segerea .

Lakini pia, nilitembelewa na viongozi wakuu wengi wa jeshi la magereza nchini akiwemo kamishena mkuu Minja.Wakuu hawa wana weledi mkubwa wa kumpa mtu somo la ‘ushauri nasaha’(counselling). Wanakufutia fikra zote za uraiani (nyumbani,mitaani na ofisini) na kukurejesha mahala pa maisha yako mapya ya gerezani na kukujuza taratibu na kanuni unazopaswa kuzifuata na kuzitii.
Madaktari na manesi waliweza kuangalia kwa karibu sana afya yangu kiasi cha kulidhibiti kwa kiasi kikubwa tatizo langu la sukari ambalo limekuwa likinisumbua kwa miaka 14 sasa.



2: KESI YA UGAIDI.

HOTUBA YA WAZIRI KIVULI NA MSEMAJI MKUU WA KAMBI RASMI YA UPINZANI WIZARA YA FEDHA NA UCHUMI NDUGU KABWE ZUBERI ZITTO KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA WIZARA KWA MWAKA WA FEDHA 2012-2013.

Wednesday, June 26, 2013

HALI ILIVYO DUNIANI KOTE JUU YA AFYA YA MANDELA.


SHORT COURSE APPLICATION FORM AT MZUMBE.

SHORT COURSE AT MZUMBE ON INTERNATIONAL PROJECT MANAGEMENT.

TCRA ICT SCHOLARSHIPS APPLICATION FORMS.

TCRA ICT SCHOLARSHIPS 2013.

Scholarships for International Students in Australia, 2013/14


Macquarie University offers International Postgraduate Research Scholarships (IPRS) and additional International Macquarie University Research Excellence (iMQRES) Scholarships. Scholarships are available to citizens of a country other than Australian/New Zealand, and not an Australian Permanent Resident. Applicants must have already completed, or expect to complete in 2013 a research masters degree. All successful IPRS PhD applicants will receive 3 years of tuition fee and compulsory health cover support. The iMQRES, available for PhD candidates only, offers the same stipend plus tuition fees for up to 3 years for students enrolling in 2014. Macquarie University ranks applicants on the basis of academic merit, relevant research experience and/or potential and the University’s research priorities. Neither the IPRS nor the iMQRES cover relocation costs. Application should be submitted till 31st August 2013.
Study Subject(s): Scholarships are provided in the areas available at the Macquarie University in Australia at Masters by research degree or Doctorate by research level.
Course Level: IPRS are available for two years Masters by research degree or three years for a Doctorate by research and MQRES scheme is a Doctoral (PhD) scholarship program.
Scholarship Provider: Macquarie University in Australia.
Scholarship can be taken at: Australia

International Scholarships in Australia 2013

The University of Melbourne offers postgraduate coursework awards for international students in Australia.  To be considered for an IPCA, applicants need to have an unconditional course offer in one of the postgraduate coursework programs. 28 scholarships are offered for the duration of the course. Scholarship offer 25% to 100% of international student tuition fees (Normally IPCAs of 25% are offered). Scholarships are awarded each year based on academic merit to outstanding international students.
Study Subject(s): Scholarships are available for Masters by coursework in the faculties of: Graduate School of Business and Economics( any coursework Masters), Melbourne School of Design( any coursework Masters), Melbourne Graduate School of Education (Masters of Teaching), Melbourne School of Engineering (any coursework Masters), Graduate School of Humanities and Social Sciences( Executive Master of Arts), Melbourne School of Land and Environment(any coursework Masters), Melbourne Law School (any Melbourne Law Masters) and Melbourne Graduate School of Science (any coursework Masters) (The list of eligible courses may vary from time to time but will be regularly updated on university’s site).
Course Level: This scholarship is available for pursuing postgraduate degree level at The University of Melbourne in Australia.
Scholarship Provider: The University of Melbourne in Australia.
Scholarship can be taken at: Australia.

MAELEZO YA WAKILI WA SUGU, TUNDU LISSU KUHUSU KUITWA POLISI DODOMA MTEJA WAKE.



Kuhusu Joseph Mbilinyi 'Sugu', Mbunge wa Mbeya Mjini. Ni kweli alikuwa polisi Dodoma, alikoitwa kwa madai ya kutoa lugha ya matusi kwa Ndugu Mizengo Pinda, lakini hajaandikisha maelezo, kwa sababu 3, zifuatazo: 

1. Wakili wake, Tundu Lissu, amewaambia kuwa Polisi hawawezi kumkamata na kumhoji Mbunge Sugu, iwe ukumbini, maeneo ya bunge, au nje ya maeneo ya bunge, wakati bunge likiendelea, kutokana na parliamentary immunity aliyonayo hadi polisi watakapofuata taratibu zinazotakiwa.

2. Neno hilo wanalotuhumu kuwa ni lugha ya matusi, si tusi kwa sheria za nchi yetu, bali linaweza kutumika kwa vitu au mtu anayefanya matendo au kusema maneno yanayostahili kuitwa hivyo. 

3. Wakili wake (Tundu Lissu)kawauliza, nani mlalamikaji katika tuhuma hizo, je wamepokea malalamiko ya Ndugu Pinda mwenyewe? Majibu yalikuwa ya kigugumizi" 

Waliondoka polisi kwa makubaliano ya kurudi leo asubuhi.


BY: Tumaini Makene

Tuesday, June 25, 2013

UCHAGUZI ARUSHA WAAHIRISHWA HADI JULAI 14.

Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imesogeza mbele chaguzi za madiwani katika kata 4 zilizoathiriwa na bomu Arusha hadi Julai 14 kwa sababu sa kiusalam.

NELSON MANDELA TAABANI.

Habari zilizotufikia hivi punde kutoka Afrika Kusini zinasema Afya ya Nelson Mandela yazidi kuzorota .Familia yake yakusanyika Hospitali pretoria na kufanya kikao cha dharura kujiandaa kwa lolote litakalojiri.

WATU 4 WAMENYONGWA NIGERIA.


Wafungwa wanne wamenyongwa kusini mwa Nigeria, katika kile maafisa wanasema kuwa hukumu ya kwanza ya kunyongwa kutekelezwa kwa miaka saba.
Kamishna wa haki katika jimbo la Edo, Henry Idahagbon, aliambia waandishi wa habari kuwa wafungwa hao walinyongwa baada ya kuhukumiwa kifo kwa makosa ya wizi wa mabavu na mauaji.




Shirika la Amnesty International lilisema kuwa hatua hiyo ya kuwanyonga wafungwa ni jambo la kuhuzunisha sana kwa watetezi wa haki za binadamu nchini Nigeria.

Zaidi ya wafungwa 1,000 nchini Nigeria wanaaminika kuhukumiwa kifo .
Vyombo vya habari nchini humo vinasema kuwa Rais Goodluck Jonathan hivi karibuni aliwataka magavana wa majimbo kutia saini vibali vya hukumu ya kifo katika jitihada za serikali kupunguza visa vya uhalifu.
Bwana Idahagbon alisema kuwa wananume wanne walinyongwa katika gereza la Benin baada ya mahakama kuamuru wanyongwe siku ya Jumatatu.
Alisema kesi zote za rufaa, hazikuweza kufua dafu na hukumu zao tayari zikuwa zimetiwa saini -mbili na magavana wa Edo Governor Adams Oshiomhole, huku nyingine zikitiwa saini na magavana wa majimbo mengine.
Ikiwa itathibitishwa , hatua hii ya kunyongwa ni ishara ya kurejea kwa sheria kali ya hukumu ya kunyongwa nchini Nigeria.
Wahudumu wa magereza ndio waliotekeleza hukumu ya kunyongwa , kitengo cha serikali wala sio jimbo la Edo.
Kulikuwa na ripoti za kutatanisha kuhusu hali ya mfungwa wa tano.
Chino Obiagwu wa kitengo cha sheria na mradi wa kuwasaidia wafungwa hao alisema kuwa mwanaume huyo alinyongwa.
Hukumu ilicheleweshwa kwa muda kwa sababu za kiufundi lakini baadaye wakapashwa habari kwa njia ya barua pepe, alisema bwana Obiagwu.
Lakini bwana Idahagbon alisema mwanaume huyo hakunyongwa kwa sababu hukumu yake ilisema kuwa auawe kwa kupigwa risasi.
Hata hivyo shirika la Amnesty International limesema kuwa limepokea habari zinazoweza kuthibitisha kuwa wafungwa wanne walinyongwa mjini Benin.

source:BBC

Scholarships at Northumbria University in UK, 2013/14.

Northumbria University offers academic scholarships for international students. The scholarships are offered as a reduction in the tuition fees for the first year of study. These scholarships are for international students with high grades joining full-time courses at the university from September 2013/14 academic year onwards. Applicants must be self-funded. The deadline for applications for the 2013 Semester 1 intake is 31st July 2013 and the deadline for Semester 2 entry is 2nd December 2013.
Study Subject (s): Scholarships are provided for studying any one of the courses offered by Northumbria University in UK.
Course Level: Scholarships are available for pursuing all full-time programmes starting from undergraduate, postgraduate and research degree programmes at Northumbria University in UK.
Scholarship Provider: Northumbria University, UK

UBOMOAJI WA MAJENGO DAR KUANZA LEO.

Wakati zoezi la kubomoa majengo yote yaliyojengwa barabarani likitarajiwa kuanza hii leo,hayo hapo juu ndo mambo yanayotarajiwa kujitokeza wakati wa utekelezaji wa zoezi hilo.

BAJETI ILIYOPITISHWA JANA KWA KURA ZA NDIYO 235 NA HAPA 35 HII HAPA.

TANAPA KUSHIRIKIANA NA VYOMBO VYA HABARI KUKABILIANA NA UJANGIRI.

Waziri wa Maliasili na Utalii Mh.Balozi Khamis Kagasheki ametangaza vita dhidi ya ujangiri. Mh.Kagasheki ameyasema hayo wakati akifungua semina iliyoandaliwa na Tanzania National parks (TANAPA) na Wahariri wa habari nchini iliyofanyika Iringa jana.
"Tunatakiwa kuchukua hatua sasa.Hali inatisha na haivumiliki" alisema wakati akijibu hoja juu ya ujangiri unaofanywa juu ya Tembo ndani ya nchi.
MKURUGENZI MKUU WA TANAPA ALLAN KIJAZI AKIONGEA KWENYE SEMINA.

AJARI: BASI LA SUMRY LAUA WATU WAWILI MKOANI DODOMA.

Basi la kampuni ya mabasi ya Sumry limepata ajari na watu 2 wamekufa hapo hapo na wengine 2  kujeruhiwa.Ajari hiyo iliyotokea jana usiku ilihusisha basi la Sumry lililokuwa linatokea Bukoba kuelekea Dar baada ya kugongana na Lori mkoani Dodoma.

Monday, June 24, 2013

UMEISOMA RASIMU YA KATIBA MPYA, HII HAPA.

Walimu watangaza mgomo rasmi Nchini Kenya.


Chama cha kitaifa cha walimu nchini Kenya, kimetangaza mgomo wa kitaifa kuanzia leo baada ya serikali kukosa kuwalipa marupurupu yao.Huu ni mgomo wa saba wa walimu tangu mwaka 2007.

Mwnyekiti wa kitaifa wa chama hicho,Wilson Sossion alituhumu serikali kwa kucheza siasa na maswala yanayowahusu walimu kwani wanafahamau masaibu ya walimu na mkataba wa mwaka 1997 uliotoa ahadi ya marupurupu hayo kwa walimu.


Kulingana na makubaliano hayo, serikali inapaswa kuwalipa walimu marupurupu ya kufanya kazi katika mazingira magumu , kuwlaipia nyumba , matibabu na pesa za usafiri.
"tumedurusu mienendo ya serikali na kugundua kuwa wantumia mtindo wa kugawanya watu. Hilo halitafanya halitafaulu,'' alisema bwana Sossion
"Tumetangza kuwa mgomo wa waalimu unaanza rasmi leo, '' aliongeza bwana Sossion
Sossion pia alisema kuwa tume ya kushughulikia maswala ya walimu, haina mamlaka ya kuwaamuru walimu kutogoma au vinginevyo kwani hilo ni jukumu la Knut.
Katibu mkuu Knut, bwana Nyamu aliseama kuwa chama cha walimu kimeweka bayana matakwa yao waliyokubana na serikali mwaka 1997.
"marupurupu haya yote sharti yalipwe.Tumekwenda kwa wizara ya limu ya kuelezea malalmiko yetu,'' alisema bwana Nyamu.
"tunawaambia walimu kuwa katibu mkuu atawapa maagizo kuhusu watakachofanya wakati wa mgomo huu. Walimu waanze kwa kukabidhi majukumu yao katika shule zao leo.
Nyamu pia aliwataka walimu kuwaondoa watoto wao shuleni kwani walimu hawatakuwepo kuwafundisha.
''Kwa sasa tunaiacha serikali ifanye uamuzi , tutaketi chini na kusubiri,'' alisema Nyamu
''Wanachokitaka walimu ni pesa, na wale wanaomshauri rais wamwambie kuwa lazima walimi wapewe pesa kwani hawatazungumzia kingine ila marupurupu yao,'' alisema Sossion

Source: BBC

Postgraduate Scholarships in UK 2013/2014.


Nottingham Trent University offers International Development Office postgraduate scholarships under International Scholarship, Vietnam Scholarship and Iraq Scholarship categories. To be eligible for a scholarship applicant must be have an offer of a place at NTU. Applicant should be a new international student starting on a new course. Sponsored students are not eligible to apply. The scholarships will be awarded on the basis of academic attainments and the quality of their personal statements. Final application should be submitted till 30th July 2013.  All applications received before 30th July will be assessed in August.
Study Subject(s): Scholarships are provided for courses offered by the Nottingham Trent University, UK.

WAMILIKI WA MABASI ARUSHA & KILIMANJARO WASITISHA MGOMO.

Wamiliki wa mabasi Mikoa ya Arusha na Kilimanjaro wamesitisha mgomo wa kubeba abiria uliokuwa uanze leo kupinga magari ya Noah kuruhusiwa kubeba abiria.
Ikumbukwe kwamba kulikuwa na mvutano kati ya wamiliki wa mabasi na serikali juu ya kuruhusu Noah kutoa huduma ya kusafirisha abiria.

WATU 10 WAMEUAWA HOTELINI- PAKISTAN.


Watu 10 wameuawa katika hoteli,kaskazini mwa   Pakistan ikiwa pamoja na watalii tisa .
Watu waliokuwa na silaha waliivamia kambi moja ya  sehemu hiyo ya Nanga Parbat na kuwaua  watalii hao.
Kwa mujibu wa taarifa, waliouawa walikuwa raia wa Ukraine,Urusi na China.
Msaidizi wa watalii,mwenyeji wa sehemu hiyo pia aliuawa.
Marekani pia imethibitisha kwamba raia wake mmoja alikuwa miongoni mwa waliouawa.
Washambuliaji 15 waliojifanya kuwa ni polisi waliivamia kambi hiyo katika jimbo la Gilgit-Baltistan
Kwa mujibu wa taarifa za mashirika ya habari, Taliban wamedai kuhusika na mashambulio hayo.
Msemaji wao ameeleza kuwa watu hao wameuliwa  kulipiza kisasi kifo cha makamu kiongozi wa Taliban ,Wali ur Rehman alieuliwa katika shambulio la  mwezi uliopita lililofanywa na ndege ya Marekani inayoruka bila ya rubani.

Source: DW

KUTOKA MJENGONI DODOMA.



TANGAZO KWA WALIOPANGIWA VITUO VYA KAZI - WIZARA YA AFYA.

MWENYEKITI UVCCM TAIFA: SIAFIKI MFUMO WA SERIKALI TATU.


MWENYEKITI wa Umoja wa vijana wa chama cha mapinduzi Taifa (UVCCM), Sadifa Juma Hamisi, amepinga vikali kuwepo kwa mfumo wa serikali tatu kama inavyopendekezwa katika rasimu ya katiba.

Sadifa ameyasema hayo wakati akizungumza na wanachama wasomi wa UVCCM kutoka katika vyuo vikuu mkoani kilimanjaro katika hafla ya kuwaaga wasomi hao na ambapo pia ametunuku vyeti vya uanachama kwa wanafunzi 312 pamoja na kuwakabidhi kadi za uanachama wanachama wapya.



Scholarships at Plymouth University in UK 2013/2014.

Plymouth University is offering international student merit scholarships for all postgraduate taught programmes. International Students can apply for these scholarships. Students must have 1st class Bachelor’s degree in a relevant subject. Applicants should hold a conditional or unconditional offer for a postgraduate taught programme at the Plymouth University for September 2013 entry. The applicant should be a self funded student and not in receipt of an official Government, company or any other scholarship. The application deadline is 30th June 2013
Study Subject (s): Scholarships are offered for all postgraduate taught programmes offered by the university.
Course Level: Scholarships are available for pursuing postgraduate degree level at Plymouth University.
Scholarship Provider: Plymouth University, UK
Scholarship can be taken at: UK
Eligibility: Applicant must meet the following eligibility criteria:

Friday, June 21, 2013

HIVI NDIVYO VIBONZO VYANGU VYA WIKI.





MAFURIKO YAUA WATU ZAIDI YA 300 INDIA.

Makundi ya waokoaji yanaendelea kuwatafuta walionusurika katika mafuriko yaliotokea katika jimbo la Uttarakhand nchini India leo, huku maafisa wakisema karibu watu 300 wamekufa.
Taarifa zinasema zaidi ya watu 13,800 wamepotea na wengine 62,800 wangali wamenasa katika maeneo hayo  karibu na miji ya shughuli za  hija za  waumini wa kihindu ya  Badrinath na Kedarth.
Picha za televisheni zimeonyesha watu wakipanda mabonde, huku wakisaidiwa na wanajseshi. Hadi sasa karibu watu 56,000 wameokolewa.

Source: DW

DAVID LUHENDE AONGEZWA KATIKA KIKOSI CHA TAIFA STARS.


  NAME  DAVID LUHENDE
NATIONALITY  TANZANIA
DATE OF BIRTH  21 JANUARY 1989
HEIGHT  5’5’ INCHES
WEIGHT  63KGs
POSITION  DEFENDER
JERSEY  29
PREVIOUS CLUB  Kagera Sugar FC

Beki wa Yanga, David Luhende ameongezwa kwenye kikosi cha Taifa Stars kwa ajili ya mechi dhidi ya Uganda (The Cranes) kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Afrika kwa Wachezaji wa Ligi za Ndani (CHAN) zitakazofanyika mwakani nchini Afrika Kusini.

Kocha Kim Poulsen amesema kutokana na uamuzi huo wa kumuongeza beki huyo wa kushoto amemuondoa mchezaji mmoja kwenye kikosi chake. Mchezaji huyo ni mshambuliaji Zahoro Pazi wa JKT Ruvu.

Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager sasa itaingia kambini kwenye hoteli ya Tansoma jijini Dar es Salaam, Julai 3 mwaka huu badala ya Julai 4 mwaka huu kama ilivyokuwa imepangwa awali.

Mechi ya Uganda itachezwa Julai 13 mwaka huu, saa 9 kamili alasiri kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam wakati ile ya marudiano itachezwa wiki mbili baadaye jijini Kampala, Uganda.

Wachezaji wanaotakiwa kambini ni Aggrey Morris (Azam), Aishi Manula (Azam), Ally Mustafa (Yanga), Amri Kiemba (Simba), Athuman Idd (Yanga), Frank Domayo (Yanga), Haruni Chanongo (Simba), John Bocco (Azam), Juma Kaseja (Simba), Juma Liuzio (Mtibwa Sugar) na Kelvin Yondani (Yanga).

Wengine ni Khamis Mcha (Azam), Mrisho Ngasa (Simba), Mudathiri Yahya (Azam), Mwadini Ali (Azam), Mwinyi Kazimoto (Simba), Nadir Haroub (Yanga), Salum Abubakar (Azam), Shomari Kapombe (Simba), Simon Msuva (Yanga) na Vincent Barnabas (Mtibwa Sugar). 


BUSH NA MKEWE KUJA NCHINI MWEZI UJAO.

Rais mstaafu wa Marekani, George W. Bush na mkewe, Laura, wanatarajiwa kuwasili nchini mwezi ujao ambapo watahutubia kongamano litakalojadili wajibu wa wake za marais katika kuinua wanawake duniani.
Taasisi ya George Bush  ndiyo imeandaa kongamano  hilo litakalofanyika Dar es Salaam kuanzia Julai 2 hadi 3.
Taarifa iliyotolewa jana na taasisi hiyo kwa vyombo vya habari, ilisema kongamano hilo, litahudhuriwa pia na mke wa Rais Barack Obama wa Marekani, Michelle na  muasisi wa Taasisi ya Wanawake ya Cherie, Cherie Blair ambaye ni mke wa Waziri Mkuu wa zamani wa Uingereza, Tony Blair.
Wake wengine wa marais wa Afrika watakaohudhuria ni Mama Salma Kikwete, Chantal Campaore wa Burkina Faso, Roman Tesfaye wa Ethiopia, Maria da Luz Dai Guebuza (Msumbiji),  Penehupifo Pohamba (Namibia), Sia Nyama Koroma (Sierra Leone), Janet Museveni (Uganda) na Christine Kaseba wa Zambia.
Kongamano hilo litajikita zaidi katika kujadili masuala ya kuwekeza kwa wake, kuimarisha Afrika lakini pia wajibu wa wake za marais  kuhamasisha wanawake katika maeneo ya elimu, afya na kuwakwamua kiuchumi.
“Kongamano hili litakutanisha pamoja wake za marais, maofisa wa Serikali, mashirika binafsi, Asasi Zisizo za Serikali (AZISE) na wasomi kujadili mambo muhimu ya kuchukuliwa hatua ili kunufaisha wanawake,” ilisema taarifa hiyo.
Aidha, mada zitakazowasilishwa na kujadiliwa katika kongamano hilo ni kuinua wajasiriamali wanawake kiuchumi kupitia mafunzo na teknolojia, kupatia fursa wanawake wakulima kwa kupewa mafunzo ya kilimo cha kisasa, mafunzo kuhusu saratani ya matiti na umuhimu wa elimu kwa wanawake.
Kongamano hilo linafanyika sambamba na ujio wa Rais Obama anayetarajiwa kuwasili nchini mwanzoni mwa mwezi ujao.
Tanzania ni miongoni mwa nchi za Afrika ambazo kiongozi huyo atazuru katika ziara itakayoanza Juni 26 hadi Julai 2. Nchi nyingine ni Senegal na Afrika Kusini.
Ziara za kiongozi huyo na Bush, inafanya Tanzania mwaka huu kushuhudia ugeni wa watu mashuhuri mfululizo, baada ya Rais Xi Jiping wa China Machi 28, ambapo Tanzania ilikuwa nchi ya kwanza kutembelea Afrika tangu achaguliwe kuwa Rais Machi 14.
Amani, utulivu na uimara wa mfumo wa demokrasia  ni miongoni mwa mambo yanayotajwa kuvutia viongozi hao wa kimataifa kuja nchini.
Wapo  wengine ambao katika maoni yao juu ya ujio wa viongozi hao, wamekuwa wakisema ugunduzi wa rasilimali za asili kama vile gesi, mafuta na madini ya urani ni sababu nyingine ya Tanzania kutembelewa.
Hata hivyo, Balozi wa Marekani nchini, Alfonso Lenhardt alikaririwa hivi karibuni akifafanua, kwamba ziara ya Obama haina ajenda yoyote ya kuchukua rasilimali za Tanzania, bali ni ya uhusiano wa kiuchumi kati ya nchi hizo.
 
Source:CCM Social media.

WIZARA YA AFYA - APPLICATION FORM FOR PRE-SERVICE COURSES 2013/2014.

SCHOLARSHIPS UNIVERSITY OF BREMEN - GERMAN 2013/2014.

University of  Bremen offers postdoctoral positions for German as well as international researchers in Germany. Post-doc positions are offered in two different variants: early career postdoctoral positions for a period of two years and independent postdoctoral positions for a period of four years. Career coaching and intensive counseling prepares the post-docs for their next career step. Early career postdoctoral positions offer the opportunity to face up to the scientific competition and to secure further external funding within two years. The advanced post-docs should set up new research groups by acquiring third-party-funding and gain the qualifications necessary for a scientific career as a professor. The number of positions available is shared equally between the natural and engineering sciences and the social sciences and humanities. The application deadline is 1st September 2013.
Study Subject(s): Post-doc positions are available in the areas of  the natural and engineering sciences and the social sciences and humanities. The number of positions available is shared equally between these areas.
Course Level: Positions are available for pursuing postdoctoral degree level: Early Career Postdoctoral Positions and Independent Postdoctoral Positions  at University of Bremen.
Scholarship Provider: University of Bremen, Germany

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...