Thursday, March 28, 2013

Breaking News: MBUNGE WA CHAMBANI ALIYEANGUKA JANA AFARIKI DUNIA.


Mbunge wa Chambani-Pemba Mh. Salim Hemed Khamis aliyeanguka ghafla jana katika kikao cha kamati ya Bunge Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa amefariki dunia.
Kwa taarifa zilizotufikia hivi punde, nikwamba mbunge huyo amefariki mchana huu na mpango wa kusafirisha mwili wa marehemu kuelekea visiwani Zanzibar zinafanyika.
Taarifa zaidi zitawajia kadiri tutakavyokuwa tunazidi kuzipata.

MENEJA MASOKO WA KAMPUNI YA VINGAMUZI VYA STAR TIMES APANDISHWA KIZIMBANI KWA UDANGANYIFU


Meneja Masoko wa Kampuni ya ving’amuzi ya Startimes, David Kisaka (37) amefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala, kujibu shtaka la kujipatia vitu kwa njia ya udanganyifu.

Mwendesha Mashtaka wa Serikali, Nassoro Katuga alidai mahakamani hapo kuwa mshtakiwa alitenda kosa hilo Januari 5, mwaka huu eneo la Akiba, Wilaya ya Ilala.
Katuga alidai siku hiyo ya tukio katika eneo hilo, mshtakiwa kwa njia ya udanganyifu alijipatia ving’amuzi 110 na Antena 30 za StarTimes vikiwa na thamani ya Sh8.4 milioni mali ya Jonathan Mkanaka.
Antena ya nje inayotumika na vingamuzi vya Startimes
 Mshtakiwa alikana shtaka na hakimu Joyce Minde aliahirisha kesi hiyo hadi Aprili 22, mwaka huu itakapotajwa tena. Mshtakiwa yupo nje ya dhamana baada ya kupata wadhamini wawili wa kuamina ambao walisaini bondi ya Sh6 milioni.

Habari  hii ni kwa hisani ya Mwananchi.

NAIBU WAZIRI ATETEA VITI MAALUM VISIONDOLEWE

Naibu Waziri wa  Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Ummy Mwalimu, ametilia shaka pendekezo la kuondolewa kwa nafasi ya Viti Maalumu Katiba Mpya.
Alisema kitendo hicho kinaweza kukwamisha malengo ya milenia  na yale ya itifaki ya jinsia na maendeleo katika  nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (Sadc) ya kuwa na uwakilishi wa asilimia 50  ya wanawake  bungeni.
Naibu  waziri huyo alisema kama  nafasi hizo zitatolewa, kuna ulazima wa katiba kutamka wazi namna ambavyo itahakisha kuwa wanawake wanapata nafasi za uongozi katika ngazi zote za serikali. Alitolea mfano katiba ya Kenya ambayo inaeleza bayana namna viongozi wanawake wanavyopatikana katika nchi hiyo.
Alisema hayo katika kongamano la waandishi  wa habari na mashirika yasiyokuwa  ya kiserikali yanayojihusisha na  masuala ya kijinsia, jijini Dar es Salaam jana.
Kongamano hilo  lilikuwa na lengo la kutathimi itifaki ya  malengo 28 ya kijinsia ya Sadc ifikapo 2015.
Naibu waziri huyo aliwataka waandishi wa habari na wanaharakati, kuhakikisha kuwa masuala ya ujinsia yanafafanuliwa kwa kiasi kikubwa katika rasimu ya Katiba Mpya inayotarajiwa kuwasilishwa juni mwaka huu na Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba.
Pia aliwataka waandishi kutumia  wanawake kama vyanzo vya  habari  kwa sababu takwimu zinaonyesha  ni asilimia 21 tu wanawake ndio wanatoa sauti katika vyombo mbalimbali vya habari hapa nchini.

Habari hii ni kwa hisani ya Mwananchi.

TETE BEACH PUB KUWAKA MOTO PASAKA HII NA Y2K SOUND

Sikukuu ya Pasaka Y2K SOUND MOROGORO itawasha moto katika viwanja vya Tete Beach Pub iliyoko Kihonda- Mazimbu road.

MaDj waliobobea wa Y2K Sound akiwemo Dj.R,Dj.Shebi zee, Dj.Parein watakuwa wanabengisha na kuwaburudisha wakazi wa Morogoro.

Katika burudani hiyo, mtu atahitajika kununua kinywaji tuu na kuendelea kuburudika.

MANJI NA MWALUSAKO WAJISALIMISHA MAHAKAMA KUU

Mwenyekiti wa Yanga Yusuph Manji akiongea na waandishi wa habari
 MWENYEKITI wa Yanga, Yusuph Manji na Katibu wake, Laurence Mwalusako, wamejisalimisha Mahakama Kuu Kitengo cha Kazi ili wajieleze kwa nini wasifungwe jela kwa kukaidi amri ya mahakama.

Viongozi hao walijisalimisha jana, mbele ya Msajili wa mahakama hiyo, Mohammed Gwaye, baada ya kutakiwa kufanya hivyo kwa sababu walishindwa kuwasilisha mahakamani hapo dhamana ya Sh 106,300,000.

Gwaye aliwaamuru kuwasilisha dhamana hiyo wakati wakisubiri hatima ya marejeo ya uamuzi uliotolewa na Kamisheni ya Usuluhishi wa Migogoro, iliyowataka Yanga kuwalipa wachezaji waliowafukuza jumla ya Sh 106,300,000 kwa kuvunja mikataba yao kinyume cha sheria.

Wachezaji hao ni Steven Malashi na Wisdom Ndlovu kutoka Malawi, waliochukuliwa na Yanga kwa mkataba wa miaka miwili wakati wakijiandaa kwa kipindi cha Ligi Kuu.

Malashi na Ndlovu walikimbilia Kamisheni ya Usuluhishi, mgogoro wao ulisikilizwa huku Yanga wakigoma, ambapo Mahakama iliamuru Ndlovu alipwe Sh milioni 57, zikiwa ni mishahara ya miaka miwili, Sh 1,800,000 gharama za usafiri kutoka Malawi, Sh milioni 20 fidia, wakati Malashi aliamuliwa kulipwa Sh milioni 18 za mshahara wa miaka miwili, Sh milioni 10 fidia na Sh 500,000 fedha zake za usajili zilizobaki kwa mwaka 2009 na 2010.

Msajili wa Mahakama Kuu Kitengo cha Kazi, Mohammed Gwaye, alitoa uamuzi wa maombi hayo Februari 4 mwaka huu, akiamuru Yanga kuwasilisha fedha hizo mahakamani wakati wakisubiri hatima ya marejeo, lakini hawakufanya hivyo hadi ilipotolewa amri ya kuitwa mahakamani kueleza kwa nini wasifungwe jela kwa kushindwa kutekeleza amri ya mahakama.

Manji na Mwalusako walifika mbele ya Msajili Gwaye kwa ajili ya kujieleza kwa nini wasifungwe, lakini msajili hakuwapa nafasi ya kuwasikiliza wala kuhoji kwa sababu jalada mama la kesi hiyo liko Mahakama ya Rufaa.

Katika kiapo kilichoapwa na Mwalusaka, anadai kwamba msuluhishi wakati akitoa uamuzi hakutilia maanani nafasi ya Yanga, kwani haina mali za kuiwezesha kulipa fedha hizo, hivyo wanaomba uamuzi ubatilishwe.

Habari hii ni kwa hisani ya Mtanzania.

KARDINALI PENGO AWATUPIA LAWAMA POLISI KUWA WANAFUGA UHALIFU


Mwadhamu Polycarp Kardinali Pengo
Askofu Mkuu wa Jimbo Katoliki la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo amelitupia lawama Jeshi la Polisi kwa kile alichosema kwamba limeshindwa kuzuia vitendo vya uvunjifu wa amani na mauaji ya watu wasiokuwa na hatia.

Kiongozi huyo akiongelea upepelezi wa mauaji ya Padri Evarist Mushi wa Zanzibar aliyepigwa risasi mwezi uliopita alisema, “Siwezi kusema naridhika au siridhiki lakini tulitegema kwamba polisi wangetegua kitendawili cha wauaji wa padri huyo.”
Mazishi ya Padre Evarist Mushi.
Kardinali Pengo alisema Serikali haipaswi kusema wanaovuruga amani ni wahuni wakati hilo ni jukumu lake kuhakikisha inadumisha amani. Pengo alikuwa akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam wakati akitoa salamu za Pasaka.

“Watu wanaharibiwa mali zao, watu wanapoteza uhai wao, Serikali haiwezi kukaa pembeni na kufikiri ni kauli za viongozi wa dini peke yao, viongozi wa dini hawana jeshi au hawawezi kukamata watu, Serikali ndiyo wana jukumu hilo kuhakikisha wanaingilia kati,” alisema Pengo na kuongeza:

“Wengine wanasema si mapambano ya dini ya Kikristu na Waislamu ila ni wahuni wachache wanajichukulia madaraka, lakini lolote liwavyo Serikali haiwezi kukwepa majukumu yake, hatuwezi kutegemea nchi itawaliwe na wahuni kama vile Serikali haipo.”

Kuhusu Padri Mushi aliyepigwa risasi na watu wasiojulikana wakati akijiandaa kwenda kwenye misa huko Zanzibar, Pengo alisema:
“Watanzania tungeambiwa zimechukuliwa hatua zipi na aliyehusika na mauaji hayo ni nani, lakini hali inayoonekana sasa hatujui.”
Aliongeza: “Siyo mimi wala Askofu wa Zanzibar (Augostino Shao) au askofu yeyote anaweza kukwambia kuwa kuna mtu amekamatwa, ila inaonekana kama mambo yanataka kuisha kimyakimya na kufanya hivyo haiwezi kuwa chimbuko la amani.”
Kardinali Pengo alisema vyombo vya kulinda amani vinapokuwa chimbuko la kuharibu amani kwa vyovyote nchi yoyote duniani haiwezi kuendelea.
Alisema kunahitajika kukutanishwa kwa pande zote mbili za Wakristu na Waislamu, lakini akatoa angalizo kwa kubainisha mambo mawili ambayo yanahitajika kuzingatiwa ili kufikia mwafaka.

Alisema pande zote mbili watu wakitaka kujadiliana ni lazima kila upande uwe tayari kujadiliana na kupokea ukweli sambamba na kusema ukweli na siyo kupotosha ukweli kwa masilahi binafsi.

“Pili kila upande uwe na mawazo kwamba upande wa pili una nia njema, lazima watu wawe tayari kuwasiliana kuwa upande wa pili una nia njema, lakini kinyume na hapo itakuwa bure na kudanganyana na mambo yataendelea kuwa mabaya zaidi,” alisema Kardinali Pengo.
Kuhusu kuwapo kwa taarifa kwamba katika mkesha wa Pasaka kuna watu watafanya vurugu, alisema haogopi kwani vyombo vya usalama vina jukumu la kuhakikisha raia wanakuwa salama.
IGP Said Mwema
“Mimi kazi yangu si kujiandaa kushika bunduki kwani Serikali wana jukumu la kulinda amani iwe kanisani au msikitini.
“Wanatakiwa kuchukulia mazungumzo hayo ‘serious’ (makini) kwani baada ya Padri Ambrose kujeruhiwa kwa risasi walisema wataendelea na kweli ikatokea Padri Mushi akauawa. Mimi sitaacha kwenda kanisani hata kama nitaambiwa nitauawa na kama kufa nife katika kanisa langu,” alisema.

Kauli ya Polisi
 
Advera Senso Msemaji Mkuu wa Polisi

Msemaji Mkuu wa Polisi, Advera Senso alisema upelelezi wa tukio la kifo cha Padri Mushi unaedelea na kuwaomba wananchi kusubiri kujua kinachoendelea.
“Kunapotokea tukio la aina yoyote lile polisi ndiyo jukumu lao kujua chanzo na hatua za kuchukua. Tunaomba watu tuwaachie wanaohusika ili kuweza kufanya kazi hiyo vizuri na tutawaeleza kinachoendelea upelelezi utakapokamilika,” alisema Senso.

Kuhusu uvumi wa matukio ya uhalifu wakati wa Pasaka, Senso alisema wanafuatilia taarifa hizo.
“Tunawaomba wananchi ambao wanajua ni kina nani wanaeneza taarifa hizo, watupe ushirikiano ili tuwachukulie hatua kutokana na kutoa taarifa za kuhatarisha usalama wa wananchi,” alisema Senso.

Pia Novemba mwaka jana, Katibu wa Mufti wa Zanzibar, Fadhili Soraga alimwagiwa Tindikali na watu wasiojulika wakati akifanya mazoezi kwenye Viwanja vya Mwanakwerekwe.

Mapema mwezi ulipita, Mchungaji wa Kanisa la Pentekoste Assemblies of God (TAG) mkoani Geita, Mathayo Kachila aliuawa katika ugomvi wa kugombea kuchinja, katika tukio ambalo watu sita walijeruhiwa vibaya kwa mapanga.

Habari hii ni kwa hisani ya Mwananchi,Alhamisi, Machi 28,2013

Wednesday, March 27, 2013

KIJANA UMRI WA MIAKA 17 AGUNDUA PROGRAMU YA SIMU IITWAYO SUMMLY NA KUWAUZIA YAHOO

Nick D'Aloisio kijana aliyegundua programu
Ni kijana aitwaye Nick D'Aloisio aliyegundua programu ya habari kwenye simu za mkononi iitwayo SUMMLY aliyoigundua Desemba 2011. Baada ya kugundua programu hiyo ameweza kuingia mkataba na kampuni ya YAHOO na atakuwa anafanya kazi katika Kampuni hiyo huku aendelea na masomo yake ya kidato cha 6.
Hata hivyo, kwenye blogu yake,ameweza kuandika maneno yafuatayo kuhusiana na programu hiyo:-
 
" In true Summly fashion, I will keep this short and sweet.

I am delighted to announce Summly has signed an agreement to be acquired by Yahoo!. Our vision is to simplify how we get information and we are thrilled to continue this mission with Yahoo!’s global scale and expertise. After spending some time on campus, I discovered that Yahoo! has an inspirational goal to make people’s daily routines entertaining and meaningful, and mobile will be a central part of that vision.  For us, it’s the perfect fit.

When I founded Summly at 15, I would have never imagined being in this position so suddenly. I’d personally like to thank Li Ka-Shing and Horizons Ventures for having the foresight to back a teenager pursuing his dream. Also to our investors, advisors and of course the fantastic team for believing in the potential of Summly. Without you all, this never would have been possible. I’d also like to thank my family, friends and school for supporting me.

Most importantly, thank you to our wonderful users who have helped contribute to us receiving Apple’s Best Apps of 2012 award for Intuitive Touch! We will be removing Summly from the App Store today but expect our summarization technology will soon return to multiple Yahoo! products - see this as a ‘power nap’ so to speak.

With over 90 million summaries read in just a few short months, this is just the beginning for our technology. As we move towards a more refined, liberated and intelligent mobile web, summaries will continue to help navigate through our ever expanding information universe.

Sincerely,

Nick
Founder"

Hata sisi Watanzania tuige mfano wa kijana huyu na tuweze kuvumbua vitu mbali mbali.

UTATA WA ELIMU YA NAIBU WAZIRI MULUGO WAZIDI KUZUA MENGI


Imebainika kuwa mmoja wa watu ambao Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philipo Mulugo (pichani)anadaiwa kutumia jina lake kutafuta kazi ya ualimu katika Shule ya Sekondari ya Southern mkoani Mbeya ni Mhadhiri katika Chuo Kikuu kishiriki cha elimu Mkwawa (Muce), kilichopo mkoani Iringa.

Mhadhiri huyo ni Dick Aron Mulungu ambaye alisoma na Mulugo katika Shule ya Sekondari ya Songea Wavulana kati ya 1994 na 1996 na alijiunga na shule hiyo baada ya kuhitimu kidato cha nne katika Shule ya Sekondari ya Kafule, ambayo iko mkoani Mbeya.

Taarifa zinaonyesha kuwa Mulungu alijiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na kupata Shahada ya kwanza katika Elimu (BA Education) 2001 na baadaye alisoma na kupata Shahada ya Uzamili (MA Development studies ) 2007.

Alipotafutwa kupitia simu yake ya mkononi, mahojiano yalikuwa hivi:
Mwandishi: Hallow…(mwandishi akajitambulisha)
Mulungu: Sawa, unasemaje?
Mwanishi: Nazungumza na Dick Mulungu?

Mulungu: Ndiyo mimi.
Mwandishi: Hivi unamfahamu mtu anayeitwa Hamimu Agustino?
Mulungu: Aah… hivi ulisema unaitwa nani?
Mwandishi: Si nimeshajitambulisha jina na ofisi ninayotoka?
Mulungu: Nipigie kesho naona hapa kuna kelele.

Mwandishi: Mbona nakusikia vizuri tu?
Mulungu: Nipigie baada ya nusu saa basi.
Baada ya nusu saa…….
Mwandishi: Haloo… naona nusu saa imekwisha, uko tayari kuzungumza?
Mulungu: Huyo simfahamu.
Mwandishi: Kwani wewe si ulisoma Songea Boys?

Mulungu: Ndiyo
Mwandishi: Kwa hiyo humkumbuki mtu aliyekuwa akitumia jina hilo?
Mulungu: Huyo mtu namkumbuka ndiyo.
Mwandishi: Kwa sasa yuko wapi?
Mulungu: Siwezi kujua, si unajua tumesoma siku nyingi sasa huwezi kujua mtu amekwenda wapi… ni siku nyingi mno.
Mwandishi: Ahsante.

Chuo Kikuu na siasa
Taarifa zinaonesha kuwa Waziri Mulugo alijiunga na Chuo Kikuu Huria cha Tanzania 2002 akitumia majina ya Philipo Hamimu Augustino na alisomea Shahada ya Sanaa katika Elimu (BA. Ed). Namba yake ya usajili chuoni hapo ni 08652/T.02.
Alipokuwa akiendelea na kazi ya ualimu Mulugo alianza harakati za kisiasa na ndipo alipoamua kwenda kugombea ubunge katika majimbo ya wilaya ya Chunya.

Kada wa chama cha NCCR Mageuzi wilayani Chunya, Nyawili Kalenda aliyejitambulisha kama mlezi wa siasa wa Waziri huyo alisema walifahamiana naye 2004 wakati Mulugo na rafiki yake walipokwenda kumtaka ushauri wa kugombea ubunge katika jimbo la Songwe.
Katika nakala za wasifu wake zinaonyesha kuwa 2008 alishika nafasi ndani ya CCM ambazo ni pamoja na mjumbe wa baraza la jumuiya ya wazazi wilaya ya Chunya, Katibu wa Elimu, Uchumi, Malezi na mazingira wa jumuiya ya wilaya hiyo na mjumbe wa baraza la wazazi mkoa wa Mbeya.

Kauli yake
Mulugo anasema madai hayo yamekuwa yakitolewa mara kwa mara na amekuwa akiyajibu kwa kuwaonyesha vyeti vyake halali vya shule. “Hayo madai ni ya muda mrefu, wewe sijui utakuwa mtu wa 20 kuuliza swali kama hilo. Mimi vyeti ninavyo na hata ukitaka ushahidi nitakuonyesha,” alisema Waziri Mulugo.

Licha ya kukiri kurudia darasa la saba, Waziri Mulugo alisema jina la Hamimu amekuwa akilitumia katika elimu tangu awali na kwamba hakuvunja sheria kufanya hivyo.

“Jina la Hamim ni la nyumbani Philipo ni jina langu la ubatizo, nadhani haya ni mambo ya kawaida na kweli nilipokuwa shule watu walikuwa wananifahamu kama Hamimu pia Philipo ni jina langu la ubatizo na kumbuka tukifika chuo huwa tunatumia jina la baba.

“Na pia ni kweli nilirudia shule kwa sababu wakati ule wa Mwalimu Nyerere na Mwinyi (Ali Hassan), sheria ilikuwa inaruhusu maana wanafunzi walikuwa wachache mno, fikiria katika darasa letu la saba tulimaliza watu saba tu. Baadaye sheria hiyo ilibadilishwa,” aliongeza.

Kuhusu jina la Dick Mulungu, alikiri kumfahamu mtu huyo na kwamba walisoma wote shule ya Sekondari ya Songea Boys. Hata hivyo, alipinga kutumia vyeti vyake.

 “Ni kweli Dick Mulungu tulisoma wote Songea Boys. Lakini hili jina la Mulungu ni jina letu la ukoo. Babu yangu alikuwa akiitwa Filipo Milambo Mulungu, kwa hiyo niliendelea kulitumia hivyo hivyo na hata jina la Mulugo ni letu pia,” alisema.

Taarifa hii ni kwa mujibu wa Mwananchi Jumanne,Machi 26,2013.

CHADEMA WAZIDI KUWAKOMALIA USALAMA WA TAIFA


 Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk Willibrod Slaa ameanza kuisakama Idara ya Usalama wa Taifa kuwa wanatumia mbinu mbalimbali kuwahujumu na kwamba mbinu zinazofanywa na idara hiyo ni kueneza propaganda walizodai za uongo dhidi yao.

Akizungumza jana makao makuu cha chama hicho jijini Dar es Salaam, Dk Slaa alisema: “Tumezibaini mbinu zinazofanywa na Usalama wa Taifa kwa kutumiwa na CCM kueneza propaganda za uongo dhidi yao kwa lengo la kukichafua chama, lakini haziwezi kufanikiwa kwani tayari tumegundua mbinu zao.”

“Chadema ni chama makini na hakiwezi kuyumbishwa na mtu yoyote wala idara yoyote inayotumiwa na baadhi ya watu ili kutaka kukizohofisha,” alisema Dk Slaa ambaye mara kwa mara amekuwa akilalamika kuchezewa rafu.

Hata hivyo, viongozi wanaohusika na idara hiyo akiwamo Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Utawala Bora), George Mkuchika walipotafutwa na gazeti hili kwa nyakati tofauti ili kuzungumzia tuhuma hizo za Dk Slaa, hawakuwa tayari kuzizungumzia.

Waziri Mkuchika alisema asingeweza kuzungumzia tuhuma hizi kwa kuwa hakuwa amezisikia wala hafahamu ni ujumbe upi uliomo katika kauli ya Dk Slaa.

“Mimi nimeshinda kwenye Kamati ya Bunge ya Katiba, Sheria na Utawala tangu asubuhi na sasa ndiyo natoka, kwa hiyo sijasikia hiyo kauli wala huo mkutano wa (Dk Slaa). Kwa hiyo siwezi kujibu chochote kwa sasa,” alisema Mkuchika na kuongeza:

“Nadhani tumeelewana na pengine tusubiri pindi nitakapofahamu ni kipi amekizungumza na nikafanyia uchunguzi tutaona kama kuna cha kujibu basi tutajibu wakati huo, lakini kwa sasa siwezi kusema chochote.”

Mapema gazeti hili lilimtafuta Mkurugenzi wa Usalama wa Taifa, Rashid Othman ili kuzungumzia madai hayo ya Chadema lakini mara zote simu yake ilikuwa haipatikani.

Baadaye Mwananchi iliwasiliana na Naibu Mkurugenzi wa Usalama wa Taifa, Jacky Nzoka ambaye alijibu kwa kifupi na kukata simu: “Mimi siyo msemaji tafadhali.”

Hata hivyo, katika tuhuma hizo Dk Slaa alisema mifano hai ipo kwake kwani kila wakati amekuwa akizungukwa na watu wa idara hiyo kwa malengo yao binafsi, lakini malengo yao hayawezi kufanikiwa kwani wao wapo makini katika hilo.

“Mimi kila wakati Usalama wa Taifa wamekuwa wakinizunguka zunguka kwa mambo yao binafsi wanayoyafuatilia kwangu, lakini nataka niwaambie kwamba nimewagundua na mbinu zao haziwezi kufanikiwa ila nawataka wasichoke kunifutalia na waendelee tu,” alisema.

Chadema na Sh400 milioni
Dk Slaa alikiwakilisha Chadema kusaini mkataba wa ushirikiano na Chama cha Konservative cha Denmark ili kuinua uwezo wa vijana na wanawake kisiasa.

Chama hicho kimeahidiwa kupewa Sh400 milioni kwa ajili ya kutoa mafunzo ya kujiimarisha kisiasa kwa Baraza la Vijana la chama hicho (Bavicha) na lile la Wanawake (Bawacha).

“Sisi leo tunasaini mkataba huu, lakini hatuufanyi siri kama vyama vingine vinavyofanya kwani mkataba huu upo wazi na kwamba kila mtu atakayetaka kuona atapewa,” alisema.

Alisema mafunzo hayo yatatolewa kwa watu 900 wa Bavicha na 900 wengine kutoka Bawacha na yanatarajia kuanza siku chache zijazo hadi Desemba mwaka huu yakiwa na lengo la kuwajengea uwezo wa kisiasa vijana wa Chadema na wanawake ili kuhakikisha wanaimarika kisiasa Tanzania,” alisema Dk Slaa.

Akizunguza wakati wa kusaini mkataba huo, Mwenyekiti wa Kamati ya Kimataifa ya Chama cha Conservative, Rolf Aagaard-Svendsen alisema lengo la ushirikino wao ni kuwajengea uwezo wa kisiasa vijana ili washiriki vizuri katika medani za kisiasa.

Habari hii ni kwa hisani ya Mwananchi,Jumatano,Machi 27,2013.

Tuesday, March 26, 2013

JOB VACANCY MANAGING DIRECTOR - DUWASA



 
DODOMA URBAN WATER SUPPLY AND SANITATION AUTHORITY
(DUWASA)           

TEL:  026 – 2324245              Website: www.duwasa.or.tz                                  P.O. BOX 431

FAX:  026 - 2320060                            E-mail:duwasatz@yahoo.com                                                      DODOMA     
 
JOB OPPORTUNITY FOR MANAGING DIRECTOR
Dodoma Urban Water Supply and Sanitation Authority (DUWASA) was established under section 3(I) of Cap. 272 of 1997 as repealed by section 60 of Water Supply and Sanitation Act No. 12 of 2009. DUWASA is an autonomous entity charged with the overall operations and management of water supply and sewerage disposal services in Dodoma Urban of the Municipality. The authority seeks to employ the services of a competent Managing Director to be stationed in Dodoma.

Applications are invited from suitably qualified, dynamic, experienced and performance driven Tanzanians male and female, to fill in the above mentioned vacancy.

1.0 Purpose of the Job
This job is a managerial position in which the holder is required to oversee all operations and systems of the authority and ensure they are in conformity with internal manuals and external guidelines such as Memorandum of understanding - MoU with the Ministry of Water and EWURA; performance Agreement targets, WHO and TBS Water and Waste water Standards and ISO 9001 Quality Management System requirements.

2.0 Main Duties and Responsibilities
Managing Director is the Chief Executive Officer responsible for managing, planning and coordinating Authorities’ activities. Among others he/she will be responsible for;
1.          Ensuring effective overall management and supervision of the Authority’s activities.
2.          Directing the formulation of policy proposals for consideration by the Board in relation to     physical and financial functions of the Authority.
3.       Interpreting policies laid down by the Board and ensure internal regulations and procedural instructions thereof.
4.        Implement and Monitor decisions and directives of the Board of Directors and duly report on the implementation.
5.       Prepare and submit to the Board, Authority’s annual plans,  budgets and priorities for approval.
6.       Be responsible for the implementation of the Performance Agreement as signed between the Board of Directors, Ministry of Water and EWURA; and ensuring that the Authority meets yearly goals, objectives and targets as stipulated in the agreements.
7.       Establishing and maintaining collaboration and link with key stakeholders such as the Ministry responsible for Water, EWURA, Regional Authorities, Media and Development partners to promote sustainable water and sewerage services as well as water projects investments and development of the Authority.
8.       Manage and control the Authority's financial and other resources in an efficient and cost effective manner in consultation with Board, EWURA and the parent Ministry.
9.       To oversee the organization's human resources and ensure that appropriate management structures and policies are developed and properly implemented.
10.   Reviews regularly, actual performance against plans and budgets and submits reports to the Board detailing performance with recommendations for actions necessary to correct adverse variance.
11.   Makes recommendations to the Boards for staffing level required by the Authority and ensures that effective procedures are established for recruitment, training and development of staff at all levels.
12.   Acting as the final authority for management decisions within the Authority, safeguards the Authority’s financial position and ensures that it discharges its financial obligations.
13.   Ensures that the Authority prepares and carries out an effective programme of public relations, water conservation & water protection and pricing policies.
14.   Ensuring that the Authority’s activities conform to the law, rules and regulations.
15.   Overseeing the planning and execution of new water & sewerage projects.
16.   Making recommendations to the Board for fixing water and sewerage tariffs and collect revenue thereof.
17.   Ensuring all Authority’s financial transactions are authorized and controlled in accordance with agreed procedures and the proper system of internal controls are maintained.
18.   Carrying out the functions of the Authority with due diligence
19.   Performing any other duties as may be assigned by the Board of Directors, Parent Ministry and Energy and Water Utilities Regulatory Authority (EWURA).

3.0 Minimum job requirements
3.1 Qualifications
v      The applicant must be a Tanzanian, with a Masters Degree from a recognized University in the fields of; Engineering, Water Resource Management, Economics, Finance, Commerce or Business Administration.  Management experience in water sector and administration is an added advantage.



3.2 Working experience
v      Possess at least 5 years experience in water supply and sanitation in a reputable organization of which 3 years should be in a senior position.

3.3 Key Competencies
v      He / She must have good inter-personal communication, computer skills and team work spirit
v      Must have demonstrated good leadership qualities and good financial management skills.
v      Must have ability to handle diverse human resource with prudence.
v      Must possess high levels of Initiative, Integrity, Enthusiasm, Accountability and Creativity.

3.4 Age limit
v      The applicant should be within the age between 35 and 50 years.

4.0 Terms of Employment
According to the Water Supply and Sanitation Act of 2009 section 17 sub-section 1, terms of employment will be 3 years renewable basing on the work performance.

5.0 Remunerations
This post attracts a salary at DOWA 14-15 scale and other fringe benefits of housing, transport, residential security, electricity and health insurance – depending on qualifications of the candidate.

6.0 Mode of Application
Applications are invited from candidates who meet the above mentioned requirements. Both electronic and hard copies are acceptable, attached with curriculum vitae, certified copies of academic transcripts and certificates, Names of 3 professional referees enclosing their recommendation letters and recent passport size photos. Hard copy applications can be posted or hand – delivered at the Authority’s offices. Applicants should clearly indicate their telephone numbers and email addresses for feedback. Applications should reach the undersigned not later than 4th April 2013 at 4.00 pm. Only short listed candidates will be contacted.

Applications should be marked “Application for the post of MD” on the envelope and addressed to;

Board Chairperson,
Dodoma Urban Water Supply and Sanitation Authority,
P.O. Box 431,
DODOMA.


Email Address: duwasatz@yahoo.com 

WANANCHI WA KIBAHA WALIGOMEA GARI LA HALMASHAURI LISIMWAGE TAKA

Wakazi wa Kibaha kwa Mfipa wakilisimamia gari lisimwage taka.
Wakazi wa Kibaha kwa Mfipa waliligomea gari la Halmashauri ya Mji Kibaha lenye nambari za usajili SM 3231 lisimwage taka katika eneo lao kutokana na kuwa taka hizo zinamwagwa juu ya calvat na zinasababisha kuzibisha calvat hilo na kufanya maji yajae kwenye makazi ya watu.
Gari la H/Mji lililozuiliwa kumwaga taka na wakazi wa Kibaha kwa Mfipa.
 Wakazi hao wamefikia hatua hiyo baada ya gari hilo kushindwa kwenda machimbo eneo ndiko yanakomwaga taka hizo baada ya barabara ya kwenda huko kujazwa vifusi na kusababisha magari yasiweze kupita.
Calvat la maji ya mvua
 Uchunguzi wa blogu hii umebaini kuwa maji katika calvat yanasafiri kwa taabu sana baada ya taka ngumu kujaa katika mkondo wa maji.

Monday, March 25, 2013

GARI LAFUNGA BARABARA YA DAR - MORO KWA MASAA KADHAA RUVU BAGAMOYO

Askari polisi wakisimamia usalama
Gari roli lenye namba za usajiri T451ARW liligongana na roli lenye namba za usajiri T475BNA eneo la Ruvu Wilaya ya Bagamoyo na kusababisha foleni kwa magari yanayotoka chalinze kwenda Dar na kutoka dar kwenda Chalinze.Foleni hiyo ilidumu kwa takribani muda usiopungua masaa matatu.
Foleni baada ya gari kuziba barabara
Kivutio zaidi ni pale vijana wapao 7 waliokuwa wakipakiza chokaa huku wakiwa hawana hata mask za kuzuia vumbi lisiwadhuru.
Vijana wakipakia chokaa




MAN UNITED YAFANIKIWA KUMSAINISHA BEKI WA KATI EZEQUIEL GARAY KUTOKA BENFICA.

Timu ya Manchester United imwfanikiwa kumsainisha Ezequiel Garay kutoka Benfica kwa kitita cha Paundi Mil.17.Man U na Benfica zimekubaliana kuwa Garay atahamia Old Traford majuma machache yajayo ili aweze kuichezea timu hiyo wakati wa kiangazi.

Garay mwenye umri wa miaka 26 aliyezaliwa Bosario tarehe 10.10.1986 amekuwa akizungumziwa mara kwa mara kuwa anawaniwa na Mashetani wekundu.

Thursday, March 21, 2013

KIKAO CHA KAMATI YA MAZINGIRA CHAFANYIKA CHINI YA NAIBU SPIKA UBELGIJI

Mheshimiwa Naibu Spika akiwasilisha taarifa kwenye kikao kinachoendelea Ubelgiji.
 Naibu spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh.Jobu Ndugai ameongoza kikao cha kamati ya mazingira na masuala ya jamii ya Mabunge ya Afrika, Carribian na Pacific (ACP) kinachoendelea kufanyika huko Brussels Ubelgiji.
Katika taarifa yake Mh.Ndugai amezungumzia ongezeko kubwa la watu Duniani pamoja na ukosefu wa rasilimali za kuwahudumia.
Picha na Said Yakub

WACHIMBA MADINI NA WAVUVI HARAMU WASABABISHA MAPIGANO MOROGORO

Mkuu wa kituo cha polisi cha kati Morogoro ,Mkuu wa Upelelezi Wilaya na Mkurugenzi Mtendaji wa MORUWASA wakiwa eneo la tukio bwawani Mindu
 Katika hali isiyokuwa ya kawaida wavuvi na wachimba madini haramu katika bwawa la Mindu walizua tafrani jana jioni baada ya wachimba madini watatu Andrea Michael, Juma Hassani na Yusuph Abdallah kukamatwa na Maaskari wa kampuni ya Mputa Security wanaolinda bwawa hilo.
Wachimba madini haramu waliokamatwa Mindu kutoka kulia Yusuph Abdallah,Juma Hassan na Andrea Michael
 Askari mmoja alipigwa na wavuvi baada ya kwenda kuwaondoa katika eneo lisiloruhusiwa kuvuliwa samaki, katika kujitetea wavuvi hao waliwapigia simu wenzao ambao walikuja na mapikipiki yapatayo 6 na kila pikipiki ikipakiza watu watatu watatu.
 Mkurugenzi mtendaji wa MORUWASA ilimbidi aende polisi kuchukua maaskari ili kuweza kuimarisha usalama katika bwawa hilo na wakati maaskari wanafika eneo la tukio wavamizi hao walikuwa wameshakimbia lakini walifanikiwa kupata mchimba madini mmoja aitwaye Juma Hassani na kwendanaye kituoni.
Awali Mkurugenzi mtendaji wa MORUWASA Ndg.John K.Mtaita akiongelea swala la kuzima mitambo ya maji na kusababisha mji karibu mzima kukosa maji alisema wamefikia hatua hiyo baada ya maji yaliyokuwa yakiingia kituo cha kutibia maji kuwa machafu sana na yananuka kutokana na mvua kuingiza maji machafu bwawani Mindu.
Mkurugenzi mtendaji wa MORUWASA akiongea na Chief Kingalu katika eneo la Mindu.

Waandishi wa habari wakiwahoji wachimba madini haramu waliokamatwa bwawani Mindu.


Wednesday, March 20, 2013

MVUA ZASABABISHA MITAMBO YA KUSAFISHA NA KUTIBIA MAJI KUZIMWA MOROGORO

Maji yakiwa yanamwagwa eneo la kutibia maji Mafiga.
 Mvua zinazoendelea kunyesha zimesababisha wataalam katika kituo cha kutibu na kusafisha maji Mfiga iliyochini ya Mamlaka ya majisafi na usafi wa mazingira Morogoro (MORUWASA) kuzima mitambo na kumwaga maji yaliyokuwa yanaingia mitamboni hapo kutoka katika bwawa la Mindu kutokana na maji hayo kuwa machafu sana kwa kujaa tope.
Sampuli ya maji yaliyokuwa yanatoka bwawa la Mindu na kuja sehemu ya kutibia maji Mafiga.
 Hali hii ilizidi zaidi kutokana na mvua iliyonyesha jana jioni hadi usiku iliyoingiza tope jingi sana kwenye mdomo wa bomba la kuchukulia maji katika bwawa la Mindu.Hata hivyo wataalamu hao wamesema watawasha mitambo tu mara hali ya maji itakaporejea katika hali yake ya kawaida.
Kuzimwa kwa mitambo hiyo kumeathiri wakazi wa Maorogoro wanaotegemea chanzo cha Mindu kukosa maji ambao ni zaidi ya 70%.
Bi.Getrude Salema Afisa Uhusiano wa MORUWASA.
 Akiongea na Blogu hii Afisa Uhusiano wa MORUWASA Bi. Getrude Salema amesema hali hii ni changamoto kwa MORUWASA. Hata hivyo amewasihi wakazi wa Morogoro kuwa wawe wavumilivu na kuwa maji yatakayowafikia yatakuwa salama pale tu watakapokuwa wamewasha hiyo mitambo na kuruhusu maji yaanze kuingia na kutibiwa.
Mkondo wa maji ya mvua unaongiza tope bwawa la Mindu.
Blogu hii imefanya ziara hadi Mitambo ya kutibia maji Mafiga, Bwawa la Mindu na Sehemu ambako maji ya mvua yanavuka barabara ya Iringa na kuingia bwawa la Mindu.Kilichoonekana ni uchimbaji wa madini karibu na bwawa,mifugo kutifua ardhi pamoja na kilimo ndo sababu zilizochangia tope kuwa jingi.
Maji ya mvua yakiwa yametuama kando kando ya barabara ya Iringa eneo la Mindu
Hata hivyo,kando kando ya barabara ya Iringa kumeonekana madimbwi mengi ya maji yakiwa yametuama kutokana na makaravati yanayopitisha maji ya mvua kuziba kiasi cha kusababisha maji kukaa kwa muda mrefu na mvua zinaponyesha zinasomba hayo maji hadi bwawa la Mindu.

Wafanyakazi wa MORUWASA wakiwa wameenda kujionea halihalisi ya mikondo inayoingiza maji ya  mvua bwawani.

SAMAKI WA MAJITAKA WAHISIWA KUUZWA KWA WATU MJINI MOROGORO


Katika hali ya kushangaza na kusikitisha, nikwamba vijana wenyeji wa Manispaa ya Morogoro wamekutwa wakikusanya samaki aina ya kambale katika mabwawa ya majitaka yanayotolewa tope ya Mafisa.
 Walipoulizwa wakasema wanaenda kula lakini uwalakini unakuja pale walipoonekana kukazana kukusanya samaki wengi na kwenda kuwasafisha.
 Wito wangu kwa wakazi wa Morogoro kuweni makini na samaki wanaouziwa na watu mitaani na kwa wale wenye mabucha kuweni waaminifu kwa kutonunua samaki watakao letwa kwao na vijana wa mtaani.
Na maafisa afya kuweni makini kwa kukagua samaki wanaouzwa kwenye mabucha na mitaani.

Monday, March 18, 2013

WAZIRI MKUU PINDA AONGOZA HARAMBEE MAGOMENI



WAZIRI MKUU Ndg.Mizengo Pinda ameongoza harambee ya papo kwa papo na kufanikiwa kukusanya sh. milioni 31.5 zikiwa ni ahadi na fedha taslimu kwa ajili ya ukarabati wa Kanisa Katoliki la Mashahidi wa Uganda la Magomeni, jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na waumini wa Kanisa hilo Jumapili asubuhi, Machi 17, 2013 kabla ya kuendesha harambee hiyo, Waziri Mkuu aliusifu uongozi wa Kanisa Katoliki la Magomeni kwa kuamua kufanya upanuzi wa kanisa hilo ili liweze kuhudumia waumini wengi zaidi.
“Nia yao ni nzuri sana na wameona mbali mapema. Magomeni hii ya leo si ya wakati ule, na wala haitakuwa hivi katika miaka mingine 50 ijayo. Zamani usingeweza kuona hata ghorofa moja hapa Magomeni lakini sasa hivi maghorofa hayahesabiki,” alisema.
Aliwasisitiza waumini hao kujitoa kwa ajili ya kazi ya Bwana kwa sababu hakuna sadaka ambayo ni ndogo. “Hakuna sadaka iliyo ndogo mbele ya Mungu, kikubwa ni dhamira tu. Kanisa ni letu na litajengwa na sisi waumini ili mradi kila mmoja wetu aseme Kansa hili nitalijenga,” alisisitiza.
Mapema akimkaribisha Waziri Mkuu kuzungumza na waumini hao, Baba Paroko wa kanisa hilo, Padri Sixfrious Rwechungura alisema wameanza kazi ya ukarabati tangu Agosti 15, 2011 na kwamba hadi sasa wamekwishakusanya sh. milioni 350 iliyotokana na nguvu za waumini wenyewe bila msaada wa kutoka nje.
Alisema wanahitaji kiasi cha sh. milioni 300 ili kukamilisha kazi hiyo ambayo inapaswa kukamilika katika miaka miwili ijayo ili iendane na maadhimisho ya miaka 50 ya kanisa hilo.
Katika harambee hiyo, Waziri Mkuu na mkewe Mama Tunu Pinda waliahidi kuchangia sh. Milioni 10 na kutoa sh. Milioni mbili za kianzio. Pia aliendesha mnada wa mbuzi aliyenunuliwa kwa sh. 600,000/- na mkoba ulionunuliwa kwa sh. 150,000/-.
(mwisho)

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...