Thursday, May 2, 2013

WABUNGE WAPIGANA VENEZUELA,MBUNGE MMOJA AUMIZWA VIBAYA.

Vurumai  zilizuka  kati  ya  wabunge  wa  Venezuela siku  ya Jumanne  usiku  ambapo  zilisababisha  kiasi  mbunge  mmoja  wa upinzani  kuumizwa  vibaya  na  kutokwa  na  damu.
Wabunge  wa  serikali  walianza  kuvurumisha  ngumi  baada  ya wabunge  wa  muungano  wa  upinzani  kufungua  bango  bungeni wakipinga  marufuku  iliyowekwa  baada  ya  uchaguzi , ambayo imesababisha  kuvuliwa  kwa  uwezo   wa  ubunge  kwa  wengi  wa wabunge  wa  upinzani.
Upande  wa  upinzani  umesema  kuwa  kiasi  ya  wabunge  17 ambao ni  washirika  wao  na    wabunge  watano wanaounga mkono  serikali  wamejeruhiwa. Wabunge  wanaounga  mkono serikali  walijitokeza  katika  televisheni  wakiwashutumu  wabunge wa  upinzani  kwa  kuwashambulia.

Chanzo:DW

No comments:

Post a Comment

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...